Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Machi 13
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa gazeti Mnara wa Mlinzi la Februari 15 na Amkeni! la Februari kwa kutumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu. Mwishoni mwa kila onyesho, mhubiri amwalike mwenye nyumba kwenye Ukumbusho.
Dak. 15: “Wasaidie Wengine Wafaidike na Fidia.”a Sehemu inayofuata itazungumzia zaidi jinsi tunavyoweza kutumia habari iliyo kwenye ukurasa wa 206-208 wa kitabu Biblia Inafundisha tunapowaalika watu kwenye Ukumbusho.
Dak. 20: Mlo wa Jioni wa Bwana—Maadhimisho Yanayomletea Mungu Heshima. Mazungumzo ya maswali na majibu yakitegemea ukurasa wa 206 hadi 208 wa kitabu Biblia Inafundisha. Katika utangulizi usiozidi dakika moja, onyesha jinsi mhubiri anavyoweza kuanzisha mazungumzo na mwenye nyumba kwa kusoma fungu la kwanza. Kisha bila kusoma mafungu, waulize wasikilizaji maswali yafuatayo: (fu. 2) Yesu alianzisha maadhimisho ya kifo chake lini? (fu. 3) Mlo wa Jioni wa Bwana unapaswa kuadhimishwa mara ngapi? (fu. 4) Biblia inafafanuaje maadhimisho ya Ukumbusho? (fu. 5) Tunajuaje kwamba Yesu hakugeuza mkate kuwa mwili wake na divai kuwa damu yake? (fu. 6) Mkate usiotiwa chachu unawakilisha nini? (fu. 7) Divai nyekundu inawakilisha nini? (fu. 8) Ni nani tu wanaopaswa kula mkate na kunywa divai? (fu. 9) Ukumbusho hufanywa lini kila mwaka, na kwa nini tunapaswa kuhudhuria? Zungumzia maandiko ya msingi wakati ukiruhusu. Watie moyo wasikilizaji wote wazungumzie habari hii na wanafunzi wa Biblia na wengine ambao wamewaalika kwenye Ukumbusho kwa kusoma mafungu, kuzungumzia mambo makuu, na kutumia maswali rahisi kama yale yaliyo katika sehemu hii.
Wimbo 134 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 20
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia mambo makuu katika sanduku “Mambo ya Kukumbuka Wakati wa Ukumbusho.”
Dak. 23: Jukumu la Kristo Katika Mpango wa Mungu. Hotuba inayotegemea kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova ukurasa wa 10-13. Unapozungumzia mafungu mawili ya kwanza chini ya kichwa kidogo “Jukumu la Kristo,” tumia dakika tatu au nne kupendekeza na kuonyesha jinsi ya kutumia mwaliko wa Ukumbusho. Rudia mapendekezo yaliyo kwenye Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 2006, ukurasa wa 3, fungu la 3.
Dak. 12: Twaimarishwa kwa Kuyachunguza Maandiko Kila Siku. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea dibaji ya Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2006. Ikiwa hamna kijitabu cha 2006, tumieni Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2005. Panga kuwe na onyesho la familia ikichunguza andiko la siku na maelezo yake.
Wimbo 103 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Machi 27
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi za Machi. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa gazeti Mnara wa Mlinzi la Machi 1 na Amkeni! la Machi kwa kutumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu. Pia onyesha jinsi unavyoweza kutumia mwaliko wa Ukumbusho kuwaalika watu wanaopendezwa kwenye Ukumbusho.
Dak. 10: Je, Bado Mungu ana Mamlaka Juu ya Dunia? Hotuba na onyesho inayotegemea ukurasa wa mwisho wa gazeti Mnara wa Mlinzi, Aprili 1, 2006. Tumia kila nafasi kuwaalika watu kwenye hotuba ya pekee. Hakikisha kwamba umewaalika wanafunzi wote wa Biblia kutia ndani washiriki wa familia ambao hawahudhurii funzo hilo. Watu wote ambao unajua wanapendezwa, kutia ndani wale tunaokutana nao katika utumishi wa shambani wanapaswa kupewa mwaliko huo wa pekee. Panga kuwe na onyesho kuhusu jinsi ya kutumia gazeti Mnara wa Mlinzi la Aprili 1 kumwalika mtu ambaye ameacha kutenda au kuhudhuria mikutano.
Dak. 25: “Mheshimu Yehova Katika Maisha Yako Sehemu ya 2—Jihadhari na Mapokeo Yasiyo ya Kikristo.”b
Wimbo 170 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 3
Dak. 15: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Pitia kifupi makala “Kujifunza Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?” iliyo katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 2006, ukurasa wa 6. Zungumzia ratiba ya funzo la kitabu Biblia Inafundisha. Pia onyesha jinsi unavyoweza kutumia mwaliko wa Ukumbusho kuwaalika watu wanaopendezwa kwenye Ukumbusho.
Dak. 10: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: “Wafundishe Wapole Kutembea Katika Njia ya Mungu.”c Tia ndani maelezo yaliyo katika Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 2004, ukurasa wa 16, fungu la 9.
Wimbo 93 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo kwa maswali na majibu.