Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/06 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Aprili 10
  • Juma Linaloanza Aprili 17
Huduma ya Ufalme—2006
km 4/06 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Aprili 10

Wimbo 49

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa gazeti Mnara wa Mlinzi la Machi 15 na Amkeni! la Machi kwa kutumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 6 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu. Katika onyesho moja, mhubiri atoe kitabu Biblia Inafundisha kwa mwenye nyumba ambaye amependezwa sana na ujumbe wa Biblia.

Dak. 15: “Jinsi ya Kudumisha Bidii.”a Tia ndani maelezo kutoka Mnara wa Mlinzi, Juni 15, 2002, ukurasa wa 14, fungu la 13.

Dak. 20: “Je, Unaweza Kubadili Ratiba Yako?”b Onyesha jinsi kutaniko linavyoweza kutumia habari hiyo. Taja mipango yoyote ambayo kutaniko limefanya kuhusu mahubiri ya jioni.

Wimbo 13 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Aprili 17

Wimbo 104

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Kazia mipango ambayo kutaniko limefanya kwa ajili ya hotuba ya pekee. Watie moyo wote waendelee kutumia ukurasa wa mwisho wa gazeti Mnara wa Mlinzi la Aprili 1, ikiwa linapatikana, kuwaalika kwenye Ukumbusho watu ambao huhudhuria Ukumbusho, wale tunaojifunza nao Biblia, na watu wengine wanaopendezwa. Kwa ufupi, eleza mambo mawili au matatu yaliyoonwa kuhusiana na kutumia gazeti hilo kuwaalika watu kwenye hotuba ya pekee.

Dak. 12: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 18: “Ongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo Mlangoni na kwa Kutumia Simu.”c Tia ndani onyesho fupi kuhusu yale ambayo mhubiri anaweza kusema ili kubadili mahali pa kufanyia funzo kutoka mlangoni hadi ndani ya nyumba.

Wimbo 162 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Aprili 24

Wimbo 66

Dak. 15: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Tutaendelea kutoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! mwezi wa Mei. Panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa gazeti Mnara wa Mlinzi la Aprili 1 na Amkeni! la Aprili kwa kutumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 6 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu. Baada ya maonyesho hayo, kazia makala nyingine katika magazeti hayo zinazoweza kuwapendeza watu katika eneo lenu.

Dak. 12: Hotuba ikitegemea makala “Michango Inayoufurahisha Moyo wa Mungu” katika Mnara wa Mlinzi, Novemba 1, 2005, ukurasa wa 26-30. Hii itakuwa fursa nzuri ya kupitia maazimio yoyote ambayo kutaniko limefanya kuhusiana na kazi ya ulimwenguni pote na mradi wa Jumba la Ufalme.

Dak. 18: Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji mkirudia mambo makuu katika makala “Mheshimu Yehova Katika Maisha Yako Sehemu ya 2—Jihadhari na Mapokeo Yasiyo ya Kikristo.” Ona nyongeza katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 2006.

Wimbo 191 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 1

Wimbo 211

Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi za Aprili. Zungumzia sanduku kwenye ukurasa wa 4, “Je, Wewe Huulizia Watu Wanaotaka Kujifunza?”

Dak. 10: “Onyesha Unawajali Wengine—Kwa Kuwatazama Wasikilizaji Inavyofaa.”d Tia ndani onyesho fupi la mhubiri akimtazama mtu mahali pa umma, aanzisha mazungumzo, na kumhubiria mtu huyo.

Dak. 15: Tafakari Matendo ya Yehova. (Zab. 77:12) Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea Kitabu cha Mwaka cha 2006. Zungumzia mambo yenye kutia moyo katika barua kutoka kwa Baraza Linaloongoza. (uku. 3-5) Zungumzia habari chini ya kichwa kidogo, “Kutafsiri Biblia.” (uku. 10-11) Simulia baadhi ya matukio muhimu na mambo yaliyoonwa mwaka uliopita. (uku. 6-64) Waalike wasikilizaji waeleze mambo waliyofurahia kusoma katika Kitabu cha Mwaka cha 2006. Watie wote moyo wakitumie kuwasaidia wanafunzi wa Biblia wasitawishe uthamini kwa tengenezo la Yehova.

Dak. 15: Pitia Sanduku la Swali.

Wimbo 82 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo kwa maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo kwa maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo kwa maswali na majibu.

d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo kwa maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki