Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/06 uku. 5
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma ya Ufalme—2006
Huduma ya Ufalme—2006
km 4/06 uku. 5

Matangazo

◼ Aprili na Mei: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Tunapowarudia watu wenye kupendezwa, kutia ndani wale ambao huhudhuria ukumbusho na/au mikutano mingine ya pekee lakini hawashirikiani sana na kutaniko, tutawatolea hasa kile kitabu kipya Biblia Inafundisha Nini Hasa? Lengo lako lapaswa kuwa kuanzisha funzo la Biblia kwa kutumia kitabu hicho. Juni: Toa kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu, lakini mwenye nyumba akisema hana watoto mtolee kitabu Ujuzi. Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Julai na Agosti: Yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutolewa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Mungu Anataka Tufanye Nini?, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na Tazama!—Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Huenda broshua zifuatazo zikafaa katika sehemu fulani za eneo lenu: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?

◼ Waandishi wa makutaniko wanapaswa kuwa na fomu za kutosha za Ombi la Utumishi wa Painia wa Kawaida (S-205) na Ombi la Utumishi wa Painia-Msaidizi (S-205b). Mnaweza kuagiza fomu hizo kwenye Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14). Wekeni akiba ya angalau mwaka mmoja. Kabla ya kutuma fomu za ombi la painia wa kawaida kwenye ofisi ya tawi, hakikisheni kwamba zimejazwa kikamili.

◼ Ofisi ya tawi inapaswa kuwa na anwani na namba za simu za karibuni za waangalizi-wasimamizi na waandishi wote. Ikiwa kuna mabadiliko yoyote ya anwani au namba za simu, Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko inapaswa kujaza Fomu ya Badiliko la Anwani ya Mwangalizi-Msimamizi/Badiliko la Anwani ya Mwandishi (S-29) na kuituma mara moja kwenye ofisi ya tawi. Pia fomu hiyo inapaswa kutumwa ikiwa kuna mabadiliko yoyote katika namba ya simu ya eneo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki