Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Taarifa: Mkutano wa Utumishi wa kila juma utapangwa katika Huduma Yetu ya Ufalme wakati wa miezi ya kusanyiko la wilaya. Makutaniko yanaweza kufanya mabadiliko yanayohitajiwa ili wahudhurie Kusanyiko la Wilaya la “Ukombozi Unakaribia!” Ikifaa, tumieni dakika 15 kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma linalotangulia kusanyiko ili kurudia mashauri na vikumbusho vinavyofaa hali zenu vilivyo katika nyongeza ya mwezi huu. Mwezi mmoja au miwili baada ya kuhudhuria kusanyiko, tumieni kati ya dakika 15 na 20 za Mkutano wa Utumishi (mnaweza kutumia sehemu ya mahitaji ya kwenu) kupitia mambo makuu ya programu ya kusanyiko. Hilo halitakuwa pitio la programu nzima ya kusanyiko. Badala yake, pitieni tu sehemu zinazohusiana moja kwa moja na huduma ya shambani. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wametumia habari hizo katika utumishi wao.
Juma Linaloanza Juni 12
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa gazeti Mnara wa Mlinzi la Mei 15 na Amkeni! la Mei kwa kutumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu. Katika onyesho moja, mhubiri atoe magazeti anapohubiri isivyo rasmi.
Dak. 20: “Huduma Yetu—Kazi Inayoonyesha Huruma.”a Wakati ukiruhusu, waombe wasikilizaji waeleze maandiko yaliyotajwa bila kunukuliwa.
Dak. 15: Kumtumaini “Mtumwa Mwaminifu na Mwenye Busara.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea sura ya 3 ya kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova.
Wimbo 47 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 19
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 20: Neno Linalosemwa Wakati Unaofaa Ni Jema Kama Nini! Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea gazeti Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 2006, ukurasa wa 16-19. Katika hotuba ya utangulizi, kazia faida nne za kuwapongeza wengine ambazo zimezungumziwa chini ya kichwa kidogo “Faida za Kutoa Pongezi.” Kisha waalike wasikilizaji wajibu maswali yafuatayo: Ni nani wa kwanza kabisa kustahili kusifiwa? Kwa nini waabudu wenzetu wanastahili kupongezwa inapofaa? Tuna fursa zipi za kuwapongeza wengine kutanikoni? Kwa nini inafaa kuwapongeza watu wa familia, na tunaweza kufanyaje hivyo? Umetiwa moyo au kuimarishwaje kwa kupongezwa?
Dak. 15: “Onyesha Unawajali Watu Kikweli—Kwa Kuwapongeza.”b Tia ndani onyesho fupi la mhubiri akimsikiliza kwa makini mwenye nyumba, anampongeza kwa unyoofu, kisha anaendeleza mazungumzo kwa kutumia yale ambayo mwenye nyumba alisema na kusoma andiko linalofaa.
Wimbo 96 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 26
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa gazeti Mnara wa Mlinzi la Juni 1 na Amkeni! la Juni kwa kutumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu. Baada ya kila onyesho, mhubiri auliza swali lenye kuchochea fikira linaloweza kujibiwa katika ziara itakayofuata akitumia kitabu Biblia Inafundisha.
Dak. 30: “Endeleeni Kumtarajia Yehova.”c Ishughulikiwe na mwandishi wa kutaniko. Taja kusanyiko ambalo kutaniko limepangiwa kuhudhuria. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo kuvaa beji ya kusanyiko wakati wote kwenye jiji au mji ambamo kusanyiko linafanyiwa kunaweza kutokeza fursa ya kuhubiri. Watie moyo wasikilizaji watafute fursa za kuhubiri isivyo rasmi na watumie fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43) wanapokutana na mtu anayependezwa.
Wimbo 208 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 3
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi za Juni ikiwa bado hawajafanya hivyo.
Dak. 15: “Kampeni ya Ulimwenguni Pote ya Kuwaalika Watu Kwenye Kusanyiko la Wilaya la ‘Ukombozi Unakaribia!’”d Someni mafungu yote.
Dak. 20: “Jinsi Unavyoweza Kufikia Miradi Yako ya Kiroho.”e Waombe vijana kutanikoni waeleze kuhusu miradi yao ya kiroho na yale wanayofanya ili kuifikia. Kijana mmoja au wawili wanaweza kuombwa watayarishe mapema maelezo yao.
Wimbo 30 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo kwa maswali na majibu.
d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo kwa maswali na majibu.
e Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo kwa maswali na majibu.