Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/06 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Julai 10
  • Juma Linaloanza Julai 17
  • Juma Linaloanza Julai 24
  • Juma Linaloanza Julai 31
  • Juma Linaloanza Agosti 7
Huduma ya Ufalme—2006
km 7/06 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Julai 10

Wimbo 4

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Juni 15 na Amkeni! la Juni kwa kutumia mapendekezo mengine yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au mapendekezo yanayofaa eneo lenu. Katika onyesho moja, mhubiri aonyeshe jinsi ya kumjibu kwa ustadi mtu anayesema “tayari sisi ni Wakristo hapa kwetu.”—Ona Kutoa Sababu, uku. 19.

Dak. 15: Mipango na Usimamizi Katika Kutaniko. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea sura ya 4 ya Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova.

Dak. 20: “Msaidie Mwanafunzi Athamini Sifa za Yehova Zisizo na Kifani.”a Tia ndani onyesho la jinsi ya kutumia maswali kumsaidia mwanafunzi wa Biblia kufikiria mambo yaliyo katika sanduku la pitio mwishoni mwa sura ya 1 ya kitabu Biblia Hufundisha.

Wimbo 88 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 17

Wimbo 99

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Zungumzia kifupi Mnara wa Mlinzi la Agosti 15, 2000, ukurasa wa 32. Kazia manufaa ya kuwa na ratiba ya kusoma Biblia kwa ukawaida hata tukiwa likizoni au wakati hatufanyi shughuli zetu za kawaida.

Dak. 15: Upendo na Unyenyekevu—Sifa Muhimu Katika Huduma. Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Agosti 15, 2002, ukurasa wa 18-20, fungu 13-20.

Dak. 20: “Tumwige ‘Mungu Wetu Mwenye Furaha,’ Yehova.”b Waombe wasikilizaji waeleze ni nini kimewasaidia wawe na mtazamo mzuri na wenye shangwe wanapohubiri katika eneo lenu.

Wimbo 189 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 24

Wimbo 218

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Julai 1 na Amkeni! la Julai kwa kutumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu. Baada ya kila onyesho, taja maneno ya utangulizi yaliyotumiwa kuamsha upendezi wa mwenye nyumba.

Dak. 10: “Wameweka Mfano Mzuri wa Uaminifu.” Hotuba na mambo yaliyoonwa ya mapainia wa pekee kutoka katika vichapo vyetu au wahoji mapainia wa pekee katika kutaniko lenu.—Ona Watch Tower Publications Index chini ya kichwa “Special Pioneers.”

Dak. 20: Iweni Imara na Thabiti. (1 Kor. 15:58) Hoji wahubiri wawili au watatu ambao wametumikia kwa uaminifu kwa miaka mingi. Walijifunzaje kweli? Kazi ya kuhubiri ilifanywaje walipoanza kuhubiri? Wamekabili matatizo gani? Wamepata baraka gani kwa kubaki imara kwa ajili ya ibada ya kweli?

Wimbo 12 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Julai 31

Wimbo 28

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi za Julai. Taja toleo la Agosti. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu. Tia ndani Kutoa Ripoti Sahihi ya Utumishi wa Shambani. Ona Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova ukurasa wa 85-87. Kazia jinsi ya kuhesabu marudio na mafunzo ya Biblia tunayoonyesha kwenye fomu ya S-4. Watie moyo wote watoe ripoti kwa ukawaida na wafanye hivyo upesi mwishoni mwa kila mwezi.

Dak. 20: “Sitawisha Mazoea Mazuri Ili Upate Baraka Nyingi.”c Waombe wasikilizaji waeleze kile ambacho wamefanya ili kuwa na ratiba nzuri ya kufanya mambo ya kiroho, jinsi ambavyo wameidumisha, na baraka ambazo wamepata.

Wimbo 130 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Agosti 7

Wimbo 209

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Onyesha kifupi jinsi mapendekezo ya kutoa vichapo yaliyo katika Huduma Yetu ya Ufalme yanavyoweza kubadilishwa yafaane na eneo lenu.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005, uku. 8.

Dak. 15: Mikutano Inayotuchochea Kwenye Upendo na Kazi Zilizo Bora. Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Machi 15, 2002, ukurasa wa 24-25. Mhoji mhubiri fulani na ukazie jinsi ambavyo yeye hujitahidi kuhudhuria mikutano kwa ukawaida na jinsi ambavyo amenufaika.

Dak. 20: Kuwa Wenye Ubunifu na Wenye Kubadilikana Katika Huduma Yetu. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea Mnara wa Mlinzi la Desemba 1, 2005, ukurasa wa 28-30. Toa hotuba inayotegemea mafungu 6-11, na ukazie jinsi Paulo alivyokuwa mwangalifu, mwenye kubadilikana, na mbunifu alipohubiri na kufundisha. Waombe wasikilizaji wajibu maswali ya mafungu 12-14, kupatana na hali za kwenu. Tia ndani onyesho la jinsi wahubiri wanavyoweza kubadili utangulizi wao shambani wakizingatia mahitaji, hali, na utamaduni wa watu katika eneo lenu.

Wimbo 83 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo kwa maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo kwa maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendelee na mazungumzo kwa maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki