Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/06 uku. 4
  • Sitawisha Mazoea Mazuri Ili Upate Baraka Nyingi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sitawisha Mazoea Mazuri Ili Upate Baraka Nyingi
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Habari Zinazolingana
  • Acha Mazoea Yakunufaishe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Vichwa vya Familia—Dumisheni Ratiba Nzuri ya Kiroho
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Fulizeni Kutembea kwa Maendeleo Katika Kawaida Yenye Utaratibu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Desturi Yako Ni Nini?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2006
km 7/06 uku. 4

Sitawisha Mazoea Mazuri Ili Upate Baraka Nyingi

1 Kabla ya kubatizwa, yaelekea ulijitahidi sana kusitawisha mazoea mazuri ya kufanya mambo ya kiroho kama vile kujifunza Biblia, kuhudhuria mikutano ya Kikristo, kushiriki katika huduma ya shambani, na kusali. Ulikua kiroho kwa sababu Yehova alibariki jitihada zako. Sasa labda miaka kadhaa imepita tangu ulipobatizwa. Je, bado una mazoea mazuri ya kufanya mambo ya kiroho ambayo ulikuwa nayo pale mwanzoni?

2 Changanua Mazoea Yako: Je, una mazoea ya kusoma Neno la Mungu kila siku? Tunapata baraka nyingi kama nini kwa kusoma Neno la Mungu kila siku! (Yos. 1:8; Zab. 1:2, 3) Katika Israeli la kale, kila mfalme alipaswa kusoma nakala yake mwenyewe ya Sheria “siku zote za maisha yake.” Mfalme angenufaikaje kwa kufanya hivyo? Angesitawisha moyo mnyenyekevu na kujifunza kumwogopa Yehova ili asigeuke kando kutoka kwenye amri Yake. (Kum. 17:18-20) Hali kadhalika leo, kusoma Biblia kila siku hutuwezesha kudumu tukiwa wanyoofu na wasio na hatia katika ulimwengu huu mbovu na uliopotoka. Pia hutuwezesha kuwa na vifaa kamili kwa ajili ya huduma.—Flp. 2:15; 2 Tim. 3:17.

3 Yesu alikuwa na desturi ya kwenda kwenye sinagogi, mahali ambapo Maandiko yalizungumziwa. (Luka 4:16) Bila shaka desturi hiyo ilimwimarisha ili aweze kukabiliana na majaribu ambayo yangempata. Sisi vilevile tunanufaishwa na maagizo ya kiroho na “ubadilishanaji wa kitia-moyo,” kwenye mikutano ya Kikristo. (Rom. 1:12) Kukusanyika pamoja na ndugu zetu hutusaidia kuvumilia hali ngumu tunazokabili katika siku hizi za mwisho. (Ebr. 10:24, 25) Je, bado una desturi ya kuhudhuria mikutano yote?

4 Masimulizi ya Biblia yanaonyesha kwamba mitume walihubiri habari njema “kila siku katika hekalu na nyumba kwa nyumba.” (Mdo. 5:42) Huenda tusiweze kuhubiri kila siku, lakini je, tunaweza kushiriki katika aina fulani ya huduma kila juma? Tukifanya hivyo, bila shaka tutaboresha ustadi wetu wa kutumia Neno la Mungu, na yaelekea tutapata mambo yenye kutia moyo tunapowajulisha wengine kweli za Biblia.

5 Nabii Danieli alibarikiwa sana kwa kumtumikia Yehova “daima” muda wote wa maisha yake. Hilo lilitia ndani mazoea yake ya kusali kwa Yehova kwa ukawaida. (Dan. 6:10, 16, 20) Vivyo hivyo, tukisali kwa ukawaida kwa Yehova kutoka moyoni, atatubariki kwa kutupa roho yake takatifu. (Luka 11:9-13) Isitoshe, Yehova atatujibu kwa kutukaribia, na hivyo kutuwezesha kuwa na uhusiano wa karibu pamoja naye. (Zab. 25:14; Yak. 4:8) Hiyo ni thawabu iliyoje! Hivyo basi, acheni tudumishe mazoea mazuri ya kufanya mambo ya kiroho ili tupate baraka nyingi kutoka kwa Yehova.

[Maswali ya Funzo]

1. Kwa nini inafaa kuchanganua mazoea yako ya kufanya mambo ya kiroho?

2. Tunanufaikaje kwa kusoma Biblia kila siku?

3. Tunapata baraka gani kwa kuhudhuria mikutano kwa ukawaida?

4. Kushiriki katika huduma ya shambani kila juma kunatunufaishaje?

5. Kwa nini ni muhimu kusali kwa Yehova kwa ukawaida?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki