Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Agosti 14
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Zungumzia makala “Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee.” Tangaza tarehe ya kusanyiko la pekee litakalofuata iwapo inajulikana. Panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Julai 15 na Amkeni! la Julai kwa kutumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu. Katika onyesho moja, mhubiri aonyeshe jinsi ya kumjibu kwa ustadi mtu anayesema “mimi sipendezwi na Mashahidi wa Yehova.”—Ona Kutoa Sababu, uku. 17.
Dak. 15: Unaweza Kuwa Chanzo cha Kitia-moyo. (Rom. 1:11, 12) Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Taja idadi ya mapainia wa kawaida katika kutaniko lenu. Onyesha njia ambazo tunaweza kuwatia moyo, kama vile kuwapongeza, kuzungumzia faida za huduma ya upainia, kushirikiana nao katika utumishi, kuwaalika kwenye mlo, na kuwasaidia kugharimia nauli. Waombe mapainia wa kawaida waeleze jinsi ambavyo wametiwa moyo na wengine. Ikiwa kutaniko halina mapainia wa kawaida, zungumzia jinsi tunavyoweza kuwatia moyo wale ambao hufanya upainia msaidizi.
Dak. 15: Ni Wakati Gani Urafiki Shuleni Huvuka Mipaka? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea ukurasa wa 17-19 wa Amkeni! la Aprili 2006. Waombe wasikilizaji ambao wamelelewa katika familia za Kikristo waeleze jinsi wazazi wao walivyowatayarisha kukabiliana na matatizo na kufuata kanuni za Biblia shuleni. Unaweza kupanga mapema mmoja au wawili wajitayarishe kutoa maelezo.
Wimbo 164 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 21
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Zungumzia makala “Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko,” na utangaze tarehe za kusanyiko la mzunguko litakalofuata iwapo zinajulikana.
Dak. 15: Nufaika Kutokana na Funzo la Mnara wa Mlinzi na Mkutano wa Watu Wote. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, ukurasa wa 59 hadi kichwa kidogo kwenye ukurasa wa 64.
Dak. 20: Panga Sasa Kuwa Painia-Msaidizi! Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Watie wahubiri moyo wajiwekee mradi wa kuwa mapainia-wasaidizi angalau mwezi mmoja katika mwaka mpya wa utumishi. (1 Kor. 9:26) Wahubiri fulani wanaweza kuchagua mwezi ulio na utendaji wa pekee, mwezi ulio na sikukuu, au ule ulio na Jumamosi na Jumapili tano. Waulize wasikilizaji: “Mmeweza kukabilianaje na hali ili mfaulu kuwa mapainia-wasaidizi? Mtu hupata baraka gani akiwa painia-msaidizi? Ikiwa ungependa kuwa painia-msaidizi lakini una shaka, kwa nini unapaswa kusali kuhusu jambo hilo? (Mdo. 4:29; 2 Kor. 4:7; Yak. 1:5) Kwa nini inafaa kuzungumzia jambo hilo pamoja na familia yenu na wengine kutanikoni ambao wanakabili hali kama zako? (Met. 15:22) Wewe unapanga kuwa painia-msaidizi lini?”
Wimbo 216 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 28
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Agosti. Panga kuwe na onyesho la jinsi ya kumtolea mtu anayepelekewa magazeti kwa ukawaida Mnara wa Mlinzi la Agosti 1 au Amkeni! la Agosti katika ziara ya kurudia. Tumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu.
Dak. 15: “Tutatoa Toleo la Pekee la Amkeni! Mwezi wa Septemba.”a Mnapozungumzia fungu la 4, tia ndani onyesho fupi la kijana akimtolea mwalimu toleo la Septemba la Amkeni!
Dak. 20: Je, Unaweza Kuanzisha Funzo la Biblia Mwezi wa Septemba? Hotuba na maonyesho. Katika Septemba, tutatia jitihada ya pekee ya kuanzisha mafunzo ya Biblia katika ziara ya kwanza tukitumia kitabu Biblia Inafundisha. Hilo lamaanisha kwamba wakati tunapomwachia mwenye nyumba kitabu, tutajaribu kuzungumzia mafungu machache pamoja naye. Panga kuwe na maonyesho mawili kwa kutumia habari inayofaa eneo lenu. Katika kila onyesho, onyesha jinsi ya kufanya mipango kamili ya kurudi na kuendeleza mazungumzo.
Wimbo 37 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 4
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: “Onyesha Unawajali Watu Kikweli—Kwa Kuhubiri Bila Ubaguzi.”b Ikiwezekana, mnapozungumzia Waroma 1:14, lilioonyeshwa mwishoni mwa fungu la 2, tia ndani maelezo mafupi kutoka katika Insight, buku la 1, ukurasa wa 255, fungu la kwanza chini ya kichwa “Barbarian.” Baada ya kuzungumzia fungu la 3, pitia hatua tatu zinazotajwa katika ukurasa wa 2 wa kijitabu Good News for People of All Nations, na uonyeshe jinsi ya kutumia kijitabu hicho kuwahubiria watu wanaozungumza lugha ya kigeni katika eneo lenu.
Wimbo 225 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.