Matangazo
◼ Toleo la Septemba: Tutatoa kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Tunapaswa kujitahidi sana kuanzisha mafunzo ya Biblia katika ziara ya kwanza. Tunapaswa kuwarudia watu wote walioachiwa kitabu hicho tukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia. Oktoba: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yakiwa pamoja. Mtu akipendezwa, tafadhali mwonyeshe broshua Endeleeni Kukesha! ili kumchochea apendezwe zaidi na Biblia. Novemba: Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Mwenye nyumba akisema hana watoto, mtolee trakti, Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? au trakti nyingine inayofaa au kitabu Ujuzi. Desemba: Tutatoa kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Au tunaweza kutoa chochote kati ya vichapo vifuatavyo: Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani, ikiwa vitabu hivyo vinapatikana katika akiba ya kutaniko.
◼ Makutaniko yanapaswa kuanza kuagiza mabuku ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ya 2006 na Watchtower Library—2006 Edition katika CD-ROM kwenye agizo la vichapo litakalofuata. Makutaniko yatapokea orodha ya lugha ambazo vichapo hivyo vinapatikana kupitia “Barua kwa Makutaniko Yote,” ambayo hutumwa kila mwezi. Kumbukeni kwamba Watchtower Library—2006 Edition imetolewa kwa ajili ya ndugu na dada waliobatizwa na inaweza kuombwa tu kupitia kutaniko.
◼ Wazee wanakumbushwa watekeleze maagizo yaliyo kwenye ukurasa wa 21-23 wa Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 1991, kuhusu watu waliotengwa au waliojitenga na ushirika ambao huenda wakataka kurudishwa.
◼ Katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba, ukurasa wa 3-6, kuna orodha ya marekebisho ambayo kila mmoja anaweza kufanya katika nakala yake ya kitabu Upeo wa Ufunuo. Kila mtu anapaswa kufanya hivyo anapojitayarisha kwa ajili ya Funzo la Kitabu la Kutaniko linaloanza juma la Januari 8, 2007.