Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/06 kur. 3-6
  • Marekebisho ya Kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Marekebisho ya Kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Vichwa vidogo
  • SURA YA 4
  • SURA YA 5
  • SURA YA 6
  • SURA YA 8
  • SURA YA 10
  • SURA YA 11
  • SURA YA 12
  • SURA YA 13
  • SURA YA 16
  • SURA YA 18
  • SURA YA 20
  • SURA YA 22
  • SURA YA 24
  • SURA YA 25
  • SURA YA 26
  • SURA YA 27
  • SURA YA 28
  • SURA YA 30
  • SURA YA 32
  • SURA YA 33
  • SURA YA 34
  • SURA YA 36
  • SURA YA 38
  • SURA YA 39
  • SURA YA 41
  • SURA YA 43
Huduma ya Ufalme—2006
km 9/06 kur. 3-6

Marekebisho ya Kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!

Mabadiliko muhimu ya kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! kilichochapishwa 1990 yameorodheshwa hapa chini. Orodha hiyo haijatia ndani mabadiliko fulani kama vile mabadiliko kuhusu idadi, ambazo zinaweza kupatikana katika Kitabu cha Mwaka cha karibuni na katika vichapo vingine.

SURA YA 4

uku. 19, ¶4, futa andiko lililotajwa mwisho: Mathayo 25:31-33

SURA YA 5

uku. 24, ¶3, badili maelezo ya chini na: * Kwa elezo refu zaidi, ona kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?, kurasa 88-92, 215-218, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

SURA YA 6

uku. 30, ¶11, mstari wa 8 kutoka juu, badili “2 Petro 3:1-3” na: 2 Petro 2:1-3

uku. 30, ¶12, badili sentensi ya sita na: Hatimaye, Konstantino Maliki Mroma aliipa dini ya “Kikristo” idhini rasmi ya Serikali, nayo hatua hiyo ikatokeza Jumuiya ya Wakristo, ambamo Kanisa na Serikali ziliunganisha kani zao katika kutawala kwa miaka elfu moja.

uku. 32, sanduku, badili fungu la kwanza na: Yesu alibatizwa na akapakwa mafuta awe Mfalme-Mchaguliwa kwenye Mto Yordani wapata Oktoba 29 W.K. Miaka mitatu na nusu baadaye, katika 33 W.K. yeye alikuja katika hekalu la Yerusalemu akatupa nje wale ambao walikuwa wakilifanya kuwa pango la wanyang’anyi. Kunaonekana kuwa na ulinganifu wa hilo katika kile kipindi cha miaka mitatu na nusu kutoka Yesu atawazwe kuwa Mfalme katika mbingu katika Oktoba 1914 mpaka kuja kwake kukagua wale waliodai kuwa Wakristo hukumu ilipoanza na nyumba ya Mungu. (Mathayo 21:12, 13; 1 Petro 4:17) Mapema katika 1918 ule utendaji wa Ufalme wa watu wa Yehova ulikutana na upinzani mkubwa. Ulikuwa wakati wa kutahini duniani pote, na wale waoga walipepetwa wakatupwa nje. Katika Mei 1918 viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walichochea kufungwa gerezani kwa maofisa wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi, lakini miezi tisa baadaye hao waliachiliwa. Baadaye, yale mashtaka ya bandia yaliyokuwa dhidi yao yaliondolewa. Tangu 1919 tengenezo la watu wa Mungu, likiwa limejaribiwa na kusafishwa, lilisonga mbele kwa bidii likatangaze Ufalme wa Yehova kwa njia ya Kristo Yesu kuwa ndilo tumaini pekee kwa aina ya binadamu.—Malaki 3:1-3.

SURA YA 8

uku. 40, ¶8, mstari wa 6 kutoka juu, badili “makosa 125” na: makosa 130

uku. 40, ¶10, badili sentensi ya mwisho na: Katika Mahakama Kuu Zaidi ya United States pekee, Mashahidi wa Yehova wameshinda maamuzi 50 yenye kupendeleka.

SURA YA 10

uku. 50, ¶11, badili maelezo ya chini na: * Ona, mathalani, ile makala “Wanawake Wakristo Waaminifu Ni Waabudu wa Mungu Wenye Thamani” katika Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 2003.

SURA YA 11

uku. 56, ¶9, badili sehemu ya pili ya fungu na: Kuhusiana na hili gazeti Mnara wa Mlinzi limetoa kitia-moyo kwa kuzungumzia habari kama vile “Endeleeni Kuthibitisha Ninyi Wenyewe Jinsi Mlivyo” na “Kuishi Si kwa Ajili Yetu Wenyewe Tena.”* Tukiwa na misaada kama hiyo ya Kimaandiko, acheni sisi tuchungue utu wetu wa ndani-ndani zaidi tunapojaribu kutembea kwa unyenyekevu na kwa sala katika ukamilifu mbele za Yehova.—Zaburi 26:1-3; 139:23, 24.

uku. 56, ¶9, badili maelezo ya chini na: * Ona Mnara wa Mlinzi Julai 15, 2005, na Machi 15, 2005.

SURA YA 12

uku. 61, ¶14, badili maelezo ya chini na: # Gazeti Mnara wa Mlinzi linalotangazwa na jamii ya Yohana, limeendelea kukazia umuhimu wa kutwaa nafasi hii na kushiriki kikamilifu kadiri iwezekanavyo katika kazi ya kuhubiri; mathalani, ona makala “Wote na Wautangaze Utukufu wa Yehova” na “Sauti Yao Ilifika Katika Dunia Yote” katika toleo la Januari 1, 2004. Katika toleo la Juni 1, 2004, katika makala “Wanaomtukuza Mungu Hubarikiwa,” mkazo uliwekwa juu ya kuingia “mlango uliofunguliwa” ndani ya utumishi wa wakati wote. Kulikuwako kilele cha mapainia 1,093,552 walioripoti utumishi kama huo katika pindi ya mwezi mmoja katika 2005.

SURA YA 13

uku. 69, ¶11, badili sentensi ya mwisho na: Karibu miaka 40 kabla ya wakati, walielekeza kwenye 1914 kuwa ule mwaka uliotiwa alama katika unabii wa Biblia kuwa ndio mwisho wa majira ya Mataifa, pamoja na matukio ya ajabu duniani.—Ufunuo 1:10.

uku. 71, ¶14, mstari wa 3, badili “zaidi ya milioni 20 katika 1988” na: zaidi ya milioni 59 katika 2006

uku. 73, ¶23, mstari wa 12 kutoka juu, futa andiko lililotajwa: Mathayo 25:31

SURA YA 16

uku. 90, ¶4, badili maelezo ya chini ya pili na: * Kupata ithibati yenye maelezo mengi ya kwamba Yesu aliingia katika Ufalme wake katika 1914, ona ukurasa wa 215-218 wa kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

uku. 90, ¶6, badili fungu hilo na: Ingawa hivyo, ni kwa nini lazima huyo Mfalme mvikwa-taji sasa hivi apande hali akienda kwenye vita? Ni kwa sababu umaliki wake unasimamishwa kukiwa na upinzani mkali kutoka kwa yule hasimu mkuu wa Yehova, Shetani Ibilisi, na wale walio juu ya dunia ambao—wakijua au pasipo kujua—wanatumikia makusudi ya Shetani. Uzawa wa Ufalme wenyewe wataka kuwe vita kuu katika mbingu. Akipiga vita kwa jina Mikaeli (linalomaanisha “Ni Nani Aliye Kama Mungu?”), Yesu anamshinda Shetani na roho waovu wake na kuwavurumisha chini kwenye dunia. (Ufunuo 12:7-12) Upandaji wenye ushindi wa Yesu unaendelea kupitia miongo ya kufungua ya siku ya Bwana wakati binadamu wenye mfano wa kondoo wanakusanywa. Ijapokuwa ulimwengu kwa ujumla ungali unalala “katika uwezo wa yule mwovu,” kwa upendo Yesu anaendelea kuchunga ndugu zake wapakwa-mafuta na waandamani wenzao, akisaidia kila mmoja apate ushindi wa imani.—1 Yohana 5:19, NW.

uku. 91, ¶9, badili sentensi ya mwisho na: Ukuzi umekuwa wenye kutokeza katika mabara ya Kikatoliki na katika nchi ambako minyanyaso ilikuwa mikali zaidi sana—kama Ujeremani, Italia, na Japani, ambamo Mashahidi wanaripoti jumla ya wahudumu wa shamba watendaji zaidi ya 600,000.—Isaya 54:17; Yeremia 1:17-19.

uku. 94, ¶18, badili fungu hilo na: Je! sisi tungeweza kuita huu kuwa ushindi wenye shangwe wa tekinolojia ya kivita? Badala ya hivyo, huo ni ushuhuda wa kwamba yule farasi mwekundu asiye na rehema yuko katika mwendo. Na mwendo huo utaishia wapi? Baadhi ya wanasayansi wanasema kwamba kuna uwezekano wa vita ya nyukilia kutokea kiaksidenti—achia mbali mteketezo mkubwa wa kinyukilia uliopangwa! Lakini kwa furaha yule Mpandaji-farasi mweupe mwenye kushinda ana fikira tofauti juu ya jambo hili.

uku. 97, ¶28, badili fungu hilo na: Lenye umaana wa kisasa hapa ni “tauni yenye kufisha.” Kufuata mikumbo ya Vita ya Ulimwengu 1, homa-mafua ya Hispania ilivuna maisha za binadamu milioni 20 katika miezi michache tu ya 1918-19. Eneo pekee duniani lililoepuka pigo hili ni kisiwa kidogo cha St. Helena. Katika mahali ambako idadi ya watu waliuawa sana na ugonjwa huu marundo ya kuni za maziko yaliwashwa ili kuchoma maiti chunguchungu. Na leo kuna tukio lenye kuogofya la ugonjwa wa moyo na kansa, na chenye kuyasababisha sana ni uchafuzi wa tumbako. Katika kile kilichoelezwa kuwa “mwongo wenye sura mbaya” wa miaka ya 1980, njia ya maisha ambayo ni ya uasi wa sheria kulingana na viwango vya Biblia iliongeza lile pigo la UKIMWI kwa ile “tauni yenye kufisha.” Katika mwaka wa 2000, iliripotiwa kwamba daktari mkuu wa Marekani alisema kwamba “huenda [UKIMWI] ndio ugonjwa mbaya zaidi wenye kuambukiza uliopata kutokea ulimwenguni.” Alisema kwamba watu milioni 52 ulimwenguni pote walikuwa na virusi vya UKIMWI, na milioni 20 kati yao tayari walikuwa wamekufa. Jinsi watu wa Yehova walivyo wenye shukrani kwamba lile shauri la hekima la Neno lake linawaepusha na uasherati na tumizi baya la damu, ambalo kupitia kwalo magonjwa mengi sana yanapitishwa leo!—Matendo 15:28, 29, NW; linga 1 Wakorintho 6: 9-11.

SURA YA 18

uku. 106, ¶7, badili fungu hilo na: Vita ya Ulimwengu 2 ilileta wimbi jingine la mabadiliko makubwa. Na vita vidogo zaidi pamoja na ugaidi wa kimataifa vinaendelea kutikisa dunia. Lile tisho la magaidi au mataifa yanayotumia silaha za maangamizi makubwa linafanya watu wengi wawe na wasiwasi.

uku. 106, badili swali namba 7-9 (b) na: Mabadiliko makubwa katika jamii ya kibinadamu wakati wa kuwapo kwa Yesu hatimaye yangetia ndani hali gani miongoni mwa wanadamu?

uku. 107, ¶9, badili sentensi ya tatu na: Zile siku zenye huzuni zilizofuata hakika zilikuwa sehemu ya utimizo wa unabii wa Yesu kuhusu kuwapo kwake, ambao ungetia ndani “huzuni kuu ya mataifa, yasijue njia ya kutokea . . . huku watu wakizirai kwa woga na taraja la vitu vinavyokuja juu ya dunia inayokaliwa.” (Luka 21:7-9, 25-31)*

uku. 107, ¶9, badili maelezo ya chini na: * Kwa zaidi ya miaka 35, kutoka 1895 mpaka 1931, maneno ya Luka 21:25, 28, 31 yalinukuliwa yakawekwa kwenye jalada la gazeti Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) dhidi ya kisetiri-nyuma cha mnara wa taa ukimulikia anga zenye dhoruba juu ya bahari yenye mchafuko.

uku. 107, ¶11, badili sentensi ya nne na: Mfumo wa ulimwengu wa Shetani umetahadharishwa kwa onyo la pote katika tufe.*

uku. 109, ¶17, futa sentensi ya pili baada ya nukuu la Ufunuo 6:12b, 13: Kinawakilisha upeo wa ile hali yenye kuleta uharibifu ambayo Yesu alikuwa ametoa unabii juu yayo mapema kwenye Mathayo 24:29.

SURA YA 20

uku. 123, ¶11, badili sentensi ya nne na: Kufikia wakati kitabu hiki kilipochapishwa, namna tofauti-tofauti za MEPS zinatumiwa katika maeneo zaidi ya 125 kuzunguka dunia, na jambo hili limesaidia kufanya iwezekane utangazaji sawia wa jarida la mara mbili kwa mwezi, Mnara wa Mlinzi, katika lugha zaidi ya 130.

uku. 128, ¶30, badili sentensi ya mwisho na: Ni sehemu ndogo tu ya aina ya binadamu, kutia na wowote kati ya 144,000 waliotiwa muhuri ambao huenda wangali wanabaki katika mnofu na umati mkubwa wa kondoo wengine ndio ‘watasimama,’ yaani, wataokoka pamoja nao.—Yeremia 35:19; 1 Wakorintho 16:13.

SURA YA 22

uku. 143, badili kichwa kidogo na: Tauni ya Nzige Leo

uku. 146, ¶16, badili sentensi zilizo baada ya nukuu la Ufunuo 9:10 na: Hiyo ingeweza kumaanisha nini? Waendapo huku na huku katika kazi yao ya Ufalme, Mashahidi wa Yehova, kwa maneno na vichapo wanatoa taarifa zenye mamlaka zinazotegemea Neno la Mungu. Ujumbe wao una mchomo wenye uchungu kama wa nge kwa sababu huonya juu ya siku ya kisasi ya Mungu inayokaribia. (Isaya 61:2) Kabla ya hiki kizazi cha sasa cha nzige wa kiroho kumaliza muda wa uhai wacho, kazi yacho iliyoamuriwa kimungu ya kujulisha wazi hukumu za Yehova itakuwa imemalizika—kwa dhara la wakufuru wote wenye shingo ngumu.

uku. 146, ¶17, badili maelezo ya chini na: * Gazeti hili lilipewa jina jipya Consolation katika 1937 na Awake! katika 1946.

uku. 147, ¶19, badili mistari 8-17 na: (Mathayo 24:3-14; Ufunuo 12:1-10, NW) Baada ya hapo, kilidondoa kutoka julisho-wazi lililochapwa London katika 1917 na likatiwa sahihi na viongozi wa kidini wanane, walioelezwa habari zao kuwa “wamo miongoni mwa wahubiri walio mashuhuri zaidi sana ulimwenguni” na waliwakilisha migawanyiko mashuhuri zaidi ya Kiprotestanti—ya Kibaptisti, Kikongrigetionali, Kipresbeteri, Kiepiskopali, na Kimethodisti.

SURA YA 24

uku. 160, ¶21, mstari wa 13, badili “watu wenye mfano wa mbuzi” na: wapinzani

uku. 160, ¶21, mstari wa 18, badili “Mathayo 25:31-34, 41, 46” na: Wafilipi 1:27, 28

uku. 160, badili swali namba 21 (b) na: Ni kwa nini habari njema ni habari mbaya kwa wapinzani?

SURA YA 25

uku. 162, ¶4, badili maelezo ya chini na: * Kupata mazungumzo kamili ya hili hekalu la kiroho, ona makala “Hekalu Kubwa la Kiroho la Yehova” katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Julai 1, 1996 na “Hekalu la Kweli Moja Mahali pa Kuabudu” katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Juni 1, 1973.

uku. 162, ¶5, badili sentensi ya tatu na: Katika unabii wa Maandiko ya Kiebrania, kuhesabu kama huko kuliandaa dhamana ya kwamba haki ingetolewa kwa msingi wa viwango vikamilifu vya Yehova.

uku. 162, ¶7, badili sentensi ya pili kufuatia nukuu la Ufunuo 11:2 na: Kama tutakavyoona, rejezo hapa ni kwa miezi 42 halisi iliyoendelea kuanzia Desemba 1914 mpaka Juni 1918, wakati wote wadaio kuwa Wakristo walitiwa katika mtihani mkali.

uku. 164, ¶12, badili sentensi ya tatu na: Kwa kuongezea, mwanzoni mwa siku ya Bwana, kulikuwako wakati uliotiwa alama wa miaka mitatu na nusu ambao magumu yaliyowapata watu wa Mungu yalilingana na matukio yaliyotolewa unabii hapa—kuanzia Desemba 1914 na kuendelea mpaka Juni 1918.

uku. 165, badili maelezo kwenye picha na: Kazi ya Zerubabeli na Yoshua ya kujenga upya ilionyesha kwamba katika siku ya Bwana mianzo midogo ingefuatwa na ongezeko kubwa miongoni mwa Mashahidi wa Yehova. Imekuwa lazima kupanua sana vifaa kama hivi vinavyoonyeshwa juu, vilivyoko Brooklyn, New York, ili kusaidia kukidhi mahitaji yao

uku. 165, ¶15, mstari wa 10, badili “(Mathayo 17:1-3; 25:31 )” na: (Mathayo 17:1-3)

SURA YA 26

uku. 175, ¶12, badili maelezo ya chini na: * Tasitasi mwanahistoria Mroma anaripoti kwamba wakati Yerusalemu lilipotekwa katika 63 K.W.K. na Kneiusi Pompeiusi akaingia ndani ya patakatifu pa hekalu, alikuta pakiwa tupu. Halikuwamo sanduku la agano ndani.—Tacitus History, 5.9.

SURA YA 27

uku. 185, ¶28, badili sentensi mbili za kwanza na: Furiko hili la ukatili la mnyanyaso lilifikia kilele wakati wa Vita ya Ulimwengu 2. Katika Ulaya Mashahidi wapatao 12,000 walitiwa katika kambi za mateso za Nazi, na 2,000 hivi wakafa.

SURA YA 28

uku. 187, ¶4, badili maelezo ya chini na: * Kwa habari zaidi, tafadhali ona kurasa 165-179 za kitabu “Sikiliza Unabii wa Danieli!” kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

p. 190, ¶15, badili sentensi tatu za kwanza na: Vita hiyo ilikuwa msiba mkubwa wa kichwa kikuu cha saba cha hayawani-mwitu. Pamoja na mataifa mengine ya Ulaya, Uingereza ilipoteza vijana wayo kwa hesabu yenye kuumiza sana. Katika pigano moja pekee, lile Pigano la Mto Somme katika 1916, kulikuwa na askari-jeshi 420,000 wa Uingereza waliokufa au kupotea vitani, pamoja na 194,000 wa Ufaransa na 440,000 wa Ujeremani—jumla ya watu zaidi ya 1,000,000 waliokufa au kupotea vitani!

uku. 192, ¶22, safu ya 1, badili mstari wa 18 na: Majaribu yao yalifikia upeo katika Juni 1918,

SURA YA 30

uku. 209, ¶10, badili mstari wa 1 na: Kufikia miaka ya 1870 Wakristo wapakwa-mafuta walianza kufanya

uku. 209, badili swali namba 10 na: Ni nini kilichotukia kufikia miaka ya 1870, naye Babuloni Mkubwa alitendaje kuitikia hilo?

uku. 212, ¶23, badili sentensi ya tatu, nne, na tano na: Mara hiyo, Yesu anatii. Kwanza, kutoka 1919 kuendelea, yeye anaagiza malaika wake wamalize kazi ya kuvuna 144,000. (Mathayo 13:39, 43; Yohana 15:1, 5, 16) Halafu, kazi ya vuno la kukusanya ndani umati mkubwa wa kondoo wengine yatukia. (Yohana 10:16; Ufunuo 7:9)

SURA YA 32

uku. 231, ¶27, badili sehemu ya mwisho ya fungu kuanzia andiko la “Mathayo 24:42, 44” na: (Mathayo 24:42, 44; Luka 12:37, 40, NW ) Akirudisha mwangwi wa onyo hilo, mtume Paulo alisema: “Siku ya Yehova inakuja sawasawa kama mwivi katika usiku. Wakati wowote wanaposema: ‘Amani na usalama!’ ndipo uharibifu wa ghafula utakuwa juu ya wao papo hapo.” Shetani ndiye anayechochea mbiu zozote bandia za “amani na usalama!”—1 Wathesalonike 5:2, 3, NW.

SURA YA 33

uku. 243, ¶21, badili sentensi ya pili kutoka mwisho na: Kwa uwazi sana, huyo papa alimtaja Yesu Kristo na Ufalme wa Mungu mara chache sana katika hotuba yake.

uku. 245, ¶25, mstari wa 6 kutoka juu, badili “(Ufunuo 14:8; 17:2)” na: (Ufunuo 14:8; 17:4)

SURA YA 34

uku. 246, ¶1, badili sentensi ya pili kutoka mwisho na: Lakini njozi hiyo inakuwa uhalisi wenye kugutusha katika siku zetu.

uku. 249, ¶10, badili sentensi ya nne na: Kulingana na ripoti iliyotolewa na Taasisi ya Utafiti wa Amani ya Kimataifa, watu wapatao milioni tano walikufa kwa sababu ya vita wakati wa 1986 pekee!

uku. 250, ¶12, maelezo ya chini, badili “1981” na: 1993

uku. 251, ¶14, badili fungu na: Katika miaka ya hivi karibuni, wanasiasa wametumia maneno “amani na usalama” kuelezea mipango mbalimbali ya wanadamu. Je! jitihada hizo za viongozi wa ulimwengu zinaonyesha mwanzo wa utimizo wa andiko la 1 Wathesalonike 5:3? Au je, Paulo alikuwa akizungumzia tukio hususa na lenye kutokeza sana hivi kwamba lingetambuliwa ulimwenguni? Kwa kuwa mara nyingi unabii wa Biblia hueleweka kikamili tu baada ya kutimia au wakati unapoendelea kutimia, itatubidi tungoje tuone itakuwaje. Kwa sasa, Wakristo wanajua kwamba hata ingawa huenda ikaonekana kana kwamba mataifa yamepata amani na usalama, hakuna kitu ambacho kwa kweli kitakuwa kimebadilika. Ubinafsi, chuki, uhalifu, mvunjiko wa jamaa, ukosefu wa adili, magonjwa, huzuni, na kifo bado vitakuwapo. Ndiyo sababu si lazima wewe uongozwe vibaya na kilio chochote cha “amani na usalama,” ikiwa umeamka kuona maana ya matukio ya ulimwengu na unatii maonyo ya kiunabii katika Neno la Mungu.—Marko 13:32-37; Luka 21:34-36.

SURA YA 36

uku. 259, ¶4, badili sentensi mbili za mwisho na: Katika 1914, Yesu alipata kuwa Mfalme mbinguni, na tangu wakati huo amekuwa akitumia mamlaka juu ya dunia akiwa Mfalme na Hakimu mshirika wa Yehova. Inafaa, basi, kwamba imempasa yeye atangaze kuanguka kwa Babuloni Mkubwa.

uku. 260, ¶9, badili sentensi nne za kwanza na: Anguko la Babuloni wa kale katika 539 K.W.K. lilikuwa mwanzo wa mshuko mrefu ambao ulimalizikia katika ukiwa wake. Hali kadhalika, tangu vita ya kwanza ya ulimwengu, uvutano wa dini ya Kibabuloni umeshuka sana kwa kadiri ya tufe lote. Kufuata vita ya ulimwengu ya pili, ibada ya Shinto ya maliki ilikatazwa katika Japani.

uku. 265, ¶22, futa andiko lililotajwa mwisho:—Linga Mathayo 24:15, 16.

uku. 266, ¶28, badili sentensi ya tatu na ya nne na: Yeye atapokea maradufu ya yale aliyotoa. Hakutakuwa na rehema kwa sababu Babuloni Mkubwa hakuonyesha rehema yoyote kwa majeruhi wake.

SURA YA 38

uku. 277, ¶17, badili sentensi mbili za mwisho na: Ikiwa bado kuna wapakwa-mafuta wowote ambao wanaokoka wakiwa duniani, pasipo shaka wataingia ndani ya thawabu yao ya kimbingu upesi baada ya Kristo kukamilisha ushindi wake, wakajiunge na washiriki wenzao wa jamii ya bibi-arusi. Ndipo wakati uliowekwa na Mungu ufikapo, ndoa ya Mwana-Kondoo yaweza kutukia!

uku. 277, ¶18, badili sentensi ya kwanza na: Simulizi la kiunabii katika Zaburi 45 (NW) linaeleza utaratibu wa matukio.

SURA YA 39

uku. 281, ¶10, badili sentensi mbili za mwisho na: Na zaidi, “malaika wote” watamtumikia Yesu anapoketi juu ya kiti cha ufalme chake chenye utukufu na kuendelea kuhukumu mataifa na vikundi vya watu wa dunia. (Mathayo 25:31, 32) Hakika, katika vita hii ya kukata maneno, wakati hukumu za Mungu zinapotekelezwa mpaka mwisho, malaika wa Yesu wataandamana tena na yeye.

SURA YA 41

uku. 296, ¶5, badili sentensi tatu za kwanza na: Ni nani wanaobaki wahukumiwe baada ya dunia ya kale na mbingu ya kale kukimbilia mbali? Si mabaki wapakwa-mafuta wa 144,000, kwa maana hawa wamekwisha hukumiwa na kutiwa muhuri. Ikiwa wapakwa-mafuta wowote bado watakuwa duniani baada ya Har–Magedoni, lazima wafe muda mfupi baada ya hapo na kupokea thawabu yao ya kimbingu kwa ufufuo. (1 Petro 4:17; Ufunuo 7:2-4)

SURA YA 43

uku. 311, ¶19, badili sentensi zinazofuata andiko la “Ufunuo 11:15; 12:10” na: Katika nyakati za mwisho, roho na bibi-arusi wamekuwa wakiwaalika watu wenye mwelekeo unaofaa wanywe maji ya uhai bure. Maji ya mto huo yataendelea kupatikana kwa ajili ya watu kama hao mpaka mwisho wa mfumo huu wa mambo na, baadaye kuendelea katika ulimwengu mpya, wakati Yerusalemu Jipya ‘linapokuja chini kutoka katika mbingu kutoka kwa Mungu.’—Ufunuo 21:2, NW.

uku. 312, ¶26, badili sentensi mbili za kwanza na: Miti hiyo, ikiwa inatiliwa maji vizuri na mto, huenda kwa kuongezea ikatia ndani washiriki 144,000 wa mke wa Mwana- Kondoo. Wanapokuwa duniani hao pia wanakunywa kutokana na uandalizi wa Mungu kwa ajili ya uhai kupitia Yesu Kristo. (Isaya 61:1-3; Ufunuo 21:6)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki