Sanduku La Swali
◼ Je, inafaa kukusanya habari ambayo itatumiwa kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na kuwapa wengine?
Inaruhusiwa kufanya hivyo kwa ajili ya washiriki wa familia na marafiki kadhaa wa karibu. Hata hivyo, habari hiyo haipaswi kugawiwa watu kwa ujumla au kuuziwa wengine kwani kufanya hivyo ni kukiuka sheria zinazohusu haki ya kunukuu.—Rom. 13:1.
Katika migawo fulani kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, ni kichwa tu ambacho hutolewa; hakuna marejeo ya mahali habari hiyo inaweza kupatikana. Je, inafaa mtu fulani kutoa orodha ya marejeo au kukusanya habari ambayo huenda ikatumiwa na kuwapa wale wenye migawo kama hiyo? La. Wala si jambo linalofaa kutayarisha majibu ya maswali ya Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ili wengine watumie, kwani kufanya hivyo hakutawasaidia kukumbuka mambo muhimu. Wanafunzi wanapaswa kufanya utafiti wao wenyewe. Hiyo ni sehemu muhimu ya mazoezi ambayo Yehova hututolea kupitia shule hiyo ili kutusaidia tuseme kwa “ulimi wa waliofundishwa.”—Isa. 50:4.