Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Oktoba 9
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, toa maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Septemba 15 na Amkeni! la Septemba pamoja na trakti Habari za Ufalme Na. 37.
Dak. 15: “Wasaidie Wengine Wawe Marafiki wa Mungu.”a Waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusiana na jinsi ambavyo mfano wa wengine na sala za kutoka moyoni za wengine zilivyowasaidia kufanya maendeleo kufikia ubatizo.
Dak. 20: Jitayarishe Kugawa Habari za Ufalme Na. 37. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Pitia mipango kwa ajili ya kampeni hiyo, kama inavyoonyeshwa katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba. Wasihi wote washiriki kikamili. Watie moyo wale walio na wanafunzi wa Biblia wanaofanya maendeleo wafikirie kama wanafunzi wao wanastahili kushiriki katika kampeni hiyo wakiwa wahubiri ambao hawajabatizwa. Wazazi wanaweza kufikiria pia iwapo watoto wao wanastahili. Taja kwa ufupi matakwa yanayotajwa kwenye ukurasa wa 79-81 wa kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova.
Wimbo 221 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 16
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 20: Kunufaika na Funzo la Kitabu la Kutaniko. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, kuanzia kichwa kidogo kwenye ukurasa wa 69 hadi kichwa kidogo cha kwanza kwenye ukurasa wa 72.
Dak. 15: “Wewe Unatanguliza Nini?”b Waombe wahubiri fulani uliowachagua waeleze jinsi ambavyo wamebadili ratiba yao ili kutanguliza mambo ya Ufalme na baraka ambazo wamepata kwa kufanya hivyo.
Wimbo 172 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 23
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Ukitumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, toa maonyesho ya jinsi tunavyoweza kutoa Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1 na Amkeni! la Oktoba. Katika onyesho moja, onyesha jinsi tunavyoweza kushughulikia kizuia-mazungumzo “Kwa nini mnawatembelea watu mara nyingi?”—Ona kitabu Kutoa Sababu, uku. 20.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: “Nufaika Kikamili na Mikutano ya Utumishi wa Shambani.”c Mnapozungumzia fungu la 3, tia ndani maelezo ya Sanduku la Swali katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 2001, fungu la 4, kuhusu jinsi mambo yanavyopaswa kushughulikiwa iwapo hakuna ndugu wanaostahili kuongoza mkutano huo.
Wimbo 143 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Oktoba 30
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote watoe ripoti za utumishi wa shambani na waandike nyuma ya karatasi ya ripoti idadi ya trakti Habari za Ufalme Na. 37 ambazo walitoa.
Dak. 15: Naweza Kuwahubiria Wanashule Wenzangu Vipi? Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji yakitegemea gazeti la Amkeni! la Machi 22, 2002, ukurasa wa 10-12. Waombe wasikilizaji waeleze mambo mazuri waliyoona walipokuwa wakihubiria wanafunzi wenzao.
Dak. 20: Mambo Tuliyoona Tulipotoa trakti Habari za Ufalme Na. 37. Waombe wasikilizaji waeleze matokeo mazuri waliyopata walipokuwa wakitoa trakti Habari za Ufalme Na. 37. Taja ni kiasi gani cha eneo ambalo limehubiriwa kufikia sasa na kinachohitajika ili kulikamilisha kabisa kufikia Novemba 12. Toa onyesho la jinsi ya kufanya ziara ya kurudia ukitumia kitabu Biblia Inafundisha. Wakumbushe wahubiri warudishe trakti zozote za Habari ya Ufalme ambazo hawataweza kugawa kabla ya kampeni kwisha ili wengine wazitumie.
Wimbo 136 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 6
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 3-4 wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, onyesha jinsi ya kutoa kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu sehemu ya pili ya mwezi wa Novemba. Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu matokeo mazuri ambayo wamepata kwa kutumia kitabu hicho shambani au katika familia zao.
Dak. 15: Pitieni sehemu “Mheshimu Yehova Katika Maisha Yako Sehemu ya 1—Katika Familia” iliyo katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 2005, ukurasa wa 3-6.
Dak. 20: Kulihubiri Neno Huleta Burudisho. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji kutoka kwenye gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 15, 2002, ukurasa wa 8-9. Waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu burudisho wanalopata kwa kuhubiri. Unaweza kupanga mapema mtu mmoja au wawili watoe maelezo.
Wimbo 8 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.