Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/06 uku. 2
  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Novemba 13
  • Juma Linaloanza Novemba 20
  • Juma Linaloanza Novemba 27
  • Juma Linaloanza Desemba 4
Huduma ya Ufalme—2006
km 11/06 uku. 2

Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Juma Linaloanza Novemba 13

Wimbo 152

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, toa maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15 na Amkeni! la Oktoba. Katika mojawapo ya maonyesho, onyesha jambo tunaloweza kufanya mwenye nyumba anaposema “Tayari naijua sana kazi yenu.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, uku. 20.

Dak. 20: Wahudumu wa Habari Njema. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, ukurasa wa 77 hadi kichwa kidogo kwenye ukurasa wa 83.

Dak. 15: “Wajasiri Lakini Wenye Kufanya Amani.”a Tia ndani maelezo kutoka kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 252-253, chini ya kichwa kidogo “Wakati wa Kukubali Maoni ya Wengine.”

Wimbo 39 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 20

Wimbo 132

Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme.

Dak. 25: Kutii Amri ya Mungu ya Kujiepusha na Damu. Hotuba ikitolewa na mzee, akitumia hati iliyotolewa na ofisi ya tawi. Taja mwanzoni kwamba kadi ya DPA haipaswi kujazwa siku hiyo. Anaposoma hati hiyo, msemaji anaweza kuongeza maelezo machache ili kutia mkazo lakini hapaswi kuongeza mifano yake au maandiko mengine. Maandiko yaliyoonyeshwa yanaweza kusomwa au kutajwa kadiri wakati unavyoruhusu. Inapofaa taja mambo yaliyo kwenye sanduku “Uandalizi Mpya wa Kutusaidia Kujiepusha na Damu.” Mwandishi anapaswa kuwapa wahubiri wote waliobatizwa kadi ya DPA pamoja na “Maagizo ya Kujaza Kadi ya DPA” ili kuwawezesha kufuatana na msemaji wakati wa sehemu hii. Mwandishi anapaswa kuhakikisha kwamba kuna idadi ya kutosha ya vitambulisho.

Dak. 15: Kutoa kitabu Mtu Mkuu mwezi wa Desemba. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Wasikilizaji watoe maelezo kuhusu mambo wanayothamini katika kitabu Mtu Mkuu na mambo yaliyoonwa walipokuwa wakitoa kitabu hicho wakati uliopita. Pitia mapendekezo kutoka kwa nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2005. Toa maonyesho ya jinsi ya kutoa kitabu hicho ukitumia mapendekezo yaliyo katika nyongeza hiyo au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu.

Wimbo 203 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 27

Wimbo 111

Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango.

Dak. 10: Kujenga Kwa Umoja Ili Kumsifu Mungu. Hotuba itakayotolewa na mzee ikitegemea Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 2006, ukurasa 17-21.

Dak. 15: “Jinsi ya Kutayarisha Utoaji wa Magazeti.”b Tia ndani onyesho la dakika tatu la wahubiri wawili, labda mume na mke, wakichagua pendekezo moja la kutoa gazeti la Novemba kati ya yale yaliyo katika ukurasa wa 8 na kuamua jinsi watakavyolitumia, na kujieleza wakitumia maneno yao wenyewe. Kisha wakitumia mapendekezo yaliyo katika makala hii, watayarishe na kutoa onyesho la jinsi watakavyotoa makala ambayo wameona inafaa eneo lao.

Dak. 15: “Nina Maoni Gani Kuhusu Visehemu vya Damu na Matibabu Yanayohusisha Damu Yangu Mwenyewe?” Mazungumzo ya maswali na majibu na onyesho. Mzee atakayeshughulikia sehemu hii afuate muhtasari uliotolewa na ofisi ya tawi.

Wimbo 120 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Desemba 4

Wimbo 155

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za mwezi wa Novemba.

Dak. 15: “Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!”c Tia moyo kutaniko litumie kwa mafanikio sehemu za ziada za kitabu hicho kama vile, sanduku na picha zilizomo. Baada ya kila funzo, somo linapaswa kupitiwa kwa kutumia Biblia.

Dak. 20: Tumia Biblia Unapojibu. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea Mnara wa Mlinzi la Agosti 15, 2002, ukurasa wa 17-18, chini ya kichwa kidogo “Kupenda Kweli Tunazojifunza.” Waombe wasikilizaji watoe maelezo kwa maswali yote. Toa onyesho la mhubiri anayetumia kitabu Kutoa Sababu kutoa jibu la Kimaandiko kwa mfanyakazi mwenzake anayeuliza, “Kwa nini husherehekei Krismasi?”

Wimbo 168 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki