Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/06 uku. 7
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma ya Ufalme—2006
Huduma ya Ufalme—2006
km 12/06 uku. 7

Matangazo

◼ Toleo la Desemba: Tutatoa kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Au tunaweza kutoa chochote kati ya vichapo vifuatavyo: Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, na Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Januari 2007: Tutatoa kitabu chochote chenye kurasa 192 ambacho kina karatasi zinazobadilika rangi au kuwa manjano, au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka 1991. Pia kitabu Ujuzi au broshua Endeleeni Kukesha! inaweza kutolewa. Februari: Tutatoa kitabu Mkaribie Yehova na kitabu Ujuzi. Machi: Tutatoa kitabu Biblia Inafundisha na tutafanya jitihada ya pekee kuanzisha mafunzo ya Biblia.

◼ Mialiko ya Ukumbusho kwa ajili ya mwaka wa 2007 itatumwa hivi karibuni katika lugha ya msingi ya kila kutaniko. Ikiwa kuna lugha nyingine zinazotumiwa katika eneo lenu nanyi mngependa kupata mialiko katika lugha hizo, mnaweza kuiagiza haraka iwezekanavyo kwa kutumia Fomu ya Kuomba Fasihi (S-14). Orodha ya lugha ambazo mialiko ya Ukumbusho inapatikana itatolewa katika “Barua kwa Makutaniko Yote” ambayo hutumwa kila mwezi. Tafadhali agizeni lugha ambazo mnahitaji katika eneo lenu.

◼ Tungependa kuwakumbusha kwamba Ukumbusho wa mwaka wa 2008 utakuwa Jumamosi, Machi 22, baada ya jua kushuka. Taarifa hii imetolewa mapema ili akina ndugu waweze kufanya mapatano ya kukodi majumba mengine mahali ambapo makutaniko kadhaa yanatumia Jumba moja la Ufalme. Wazee wanapaswa kufanya mapatano na wasimamizi wa jumba watakalokodi ili kuhakikisha kwamba Ukumbusho unaadhimishwa kwa njia ya amani na kwa utaratibu bila kuvurugwa na utendaji mwingine katika jengo hilo. Kwa sababu Ukumbusho ni tukio muhimu, baraza la wazee linapaswa kumteua mzee anayestahili zaidi atoe hotuba ya Ukumbusho badala ya kupokezana zamu tu au kutumia ndugu yuleyule kila mwaka. Ikiwa kuna mzee mwenye uwezo ambaye ni mtiwa-mafuta, apewe mgawo huo.

◼ Vitabu na magazeti yote yaliyopo yahesabiwe Desemba 31, 2006 au haraka iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Hesabu hiyo ni kama ile inayofanywa kila mwezi na mratibu wa vitabu, na jumla ziandikwe kwenye fomu ya Orodha ya Vitabu (S-18). Jumla ya idadi ya magazeti yaliyopo inaweza kupatikana kutoka kwa watumishi wa magazeti. Mwandishi wa kutaniko linaloratibu anapaswa kusimamia kazi hiyo. Mwandishi na mwangalizi-msimamizi wa kutaniko linaloratibu watie sahihi fomu hiyo. Kila kutaniko linaloratibu litapokea nakala tatu za fomu ya Orodha ya Vitabu (S-18). Tafadhali tumeni nakala ya kwanza kwa ofisi ya tawi kabla ya Januari 6. Wekeni nakala ya kaboni kwenye faili zenu. Nakala ya tatu inaweza kutumiwa ili kufanyia hesabu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki