Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Aprili 9
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Watie moyo wote watazame drama kwenye DVD yenye kichwa Young People Ask—What Will I Do With My Life? ili wawe tayari itakapozungumziwa kwenye Mkutano wa Utumishi juma lijalo. Waelekeze kwenye sanduku lenye kichwa “Main Menu,” katika DVD hiyo na uwaeleze jinsi wanavyoweza kutoka sehemu moja ya DVD hiyo hadi nyingine. Mahali ambapo DVD hiyo haipatikani, tayarisheni makala yenye kichwa, “Unakadiriaje Mafanikio?” katika Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 2000 ukurasa wa 18-21. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, toa maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Machi 15 na Amkeni! la Machi. Katika onyesho moja, mhubiri aulize swali atakalojibu kwenye ziara ya kurudia.
Dak. 15: “Wote Wanaweza Kushiriki Kufanya Wanafunzi Wapya.”a Mnapozungumzia fungu la 4, waalike wasikilizaji waeleze jinsi walivyotiwa moyo na ndugu na dada kutanikoni kabla ya kubatizwa. Unaweza kupanga mapema mtu mmoja au wawili wajitayarishe kutoa maelezo.
Dak. 20: “Jifunze Biblia na Watu Wanaochukua Magazeti.”b Tia ndani onyesho fupi linalotegemea mapendekezo yaliyo kwenye fungu la 2. Wakumbushe wahubiri kwamba funzo la Biblia linaweza kuripotiwa linapokuwa limeongozwa mara mbili mara baada ya mtu huyo kuonyeshwa jinsi funzo linavyoandaliwa, na ikiwa kuna sababu za kuamini kwamba funzo hilo litaendelea.
Wimbo 43 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 16
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: “Sema Neno la Mungu Bila Woga.”c Muda ukiruhusu, waalike wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yaliyoonyeshwa.
Dak. 20: Mazungumzo ya makala yenye kichwa “Unakadiriaje Mafanikio?” katika Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 2000 ukurasa wa 18-21.d Mahali ambapo DVD zinapatikana zungumzeni pamoja na wasikilizaji mkitumia sehemu yenye kichwa “Utayatumiaje Maisha Yako?”—Sehemu ya 1. Baada ya kutoa maelezo mafupi kwenye fungu la 1 na 2, ingia moja kwa moja kwenye mazungumzo yanayotegemea maswali ya fungu la 3 hadi 4. Soma maandiko yote mawili unapozungumzia swali la 4 kwenye fungu la 3. Unapomaliza, pitia sanduku “Main Menu.” Watie moyo wote watazame “Interviews (Mahojiano)” na “Supplementary Material (Habari za Ziada)” kwenye DVD ili wajitayarishe kwa mazungumzo juma lijalo kwenye Mkutano wa Utumishi.
Wimbo 207 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 23
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Ukitumia mapendekezo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, toa maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Aprili 1 na Amkeni! la Aprili.
Dak. 10: Tazama! Nuru Ni ya Ajabu! Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Machi 15, 2007, ukurasa wa 12-14.
Dak. 25: Mzungumzie makala “Vijana, Je, Mnajitayarisha Kwa Ajili ya Wakati Ujao?” katika Mnara wa Mlinzi la Mei 1, 2004 ukurasa wa 13-18, au mahali ambapo DVD inapatikana, mzungumzie: “Utayatumiaje Maisha Yako?”—Sehemu ya 2.e Ingia moja kwa moja kwenye mazungumzo yanayotegemea maswali kwenye fungu la 5 hadi 7. Malizia kwa himizo changamfu linalotolewa kwenye fungu la 8.
Wimbo 172 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 30
Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi za mwezi Aprili.
Dak. 10: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 30: “Kutimiza Huduma Yetu ya Ufalme Tukiwa Mashahidi wa Yehova.”f
Wimbo 44 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 7
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: Mipango ya Kupata na Kudumisha Mahali pa Ibada. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea sura ya 11 ya kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova.
Dak. 20: “Watu Wasipopatikana Nyumbani.”g Itolewe na mwangalizi wa utumishi.
Wimbo 178 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
e Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
f Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
g Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.