Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/07 uku. 3
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma ya Ufalme—2007
Huduma ya Ufalme—2007
km 5/07 uku. 3

Matangazo

◼ Toleo la Mei: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Tunapowarudia watu wenye kupendezwa, kutia ndani wale ambao huhudhuria Ukumbusho na/au mikutano mingine ya pekee lakini hawashirikiani sana na kutaniko, tutajitahidi kuwatolea kitabu Biblia Inafundisha, tukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia. Juni: Kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? au Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Pia kitabu Ujuzi kinaweza kutolewa. Julai na Agosti: Yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 inaweza kutolewa: Endeleeni Kukesha!, Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je, Uamini Utatu?, Jina la,Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Huenda broshua zifuatazo zikafaa sehemu fulani za eneo lenu: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?

◼ Hundi zinazotolewa kama michango kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote katika makusanyiko ya wilaya na zile zinazotumwa kwenye ofisi ya tawi ziandikwe jina la shirika linalotambuliwa kisheria katika nchi yenu.

◼ Mabaraza ya wazee yanapaswa kupitia barua ya Julai 6, 2006 kuhusu kujitayarisha kwa ajili ya msiba na wahakikishe kwamba wana habari za karibuni za kila mhubiri. Katika maeneo ambayo hukumbwa na misiba mara kwa mara, wazee wanapaswa kuwa na habari za ziada za jinsi wanavyoweza kuwasiliana na wahubiri wakati wa dharura. Mbali na wakati wa dharura, ingefaa wahubiri wamjulishe mwangalizi wa Funzo lao la Kitabu la Kutaniko au mzee mwingine ikiwa hawatakuwapo kwa muda mrefu kama vile ikiwa watasafiri kwenda likizo au safari za kikazi, ikiwa watalazwa hospitalini, au hali nyingine kama hizo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki