Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/07 uku. 7
  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Huduma ya Ufalme—2007
Huduma ya Ufalme—2007
km 6/07 uku. 7

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatashughulikiwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Juni 25, 2007. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Mei 7 hadi Juni 25, 2007. [Taarifa: Mahali ambapo vichapo vya marejeo havijaonyeshwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]

SIFA ZA USEMI

1. Tunaweza kufanya nini kutuliza mkazo ili kuboresha sauti tunapozungumza? [be uku. 184 fu. 3-uku. 185 fu. 2]

2. Tunawezaje ‘kuwa mambo yote kwa watu wa namna zote’ katika huduma ya shambani? (1 Kor. 9:20-23) [be uku. 186 fu. 2-4]

3. Tunawezaje kuiga mfano wa Yehova wa kuwasikiliza watu wengine? (Mwa. 18:23-33; 1 Fal. 22:19-22) [be uku. 187 fu. 1-2, 5]

4. Tunaweza kutumia njia zipi kuwasaidia wengine wafanye maendeleo ya kiroho? [be uku. 187 fu. 6–uku. 188 fu. 3]

5. Kwa nini tunapaswa kujali watu kwa kuwaonyesha heshima? [be uku. 190 fu. 3, sanduku]

HOTUBA NA. 1

6. Kwa nini tunapaswa kujaribu kufikia mioyo ya wale tunaowafundisha? [be uku. 59 fu. 1]

7. Mfano wetu unawasaidiaje watu tunaowafundisha? [be uku. 61 fu. 1]

8. Tunawezaje kuboresha mazungumzo yetu nyumbani? [be uku. 62 fu. 3]

9. Ni kielelezo gani cha bidii ya moyo mkuu tunachopata katika nabii Yeremia? [si uku. 129 fu. 36]

10. Ni uhakika gani ambao Maombolezo chaeleza, hata hivyo kwa nini ni chenye mafaa katika kuonyesha ukali wa hukumu za Mungu dhidi ya waovu? [si uku. 132 fu. 13]

USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA

11. Kama vile ilivyokuwa katika kisa cha Yeremia kinachoelezwa kwenye kitabu cha Yeremia 37:21, tunahakikishiwa nini?

12. Kwa nini Baruku alisema Yehova “ameongeza huzuni juu ya maumivu yangu” na hivyo kumfanya ‘achoke,’ na mwanzoni itikio lake lilikuwaje? (Yer. 45:1-5)

13. Babiloni iliacha kukaliwa lini na kuwa “mahame yenye ukiwa”? (Yer. 50:13)

14. Ni kanuni gani kuhusu sala inayoonyeshwa waziwazi kwenye kitabu cha Maombolezo 3:8, 9, 42-45?

15. Ni nini kinachowakilishwa na gari la kimbingu linalofafanuliwa kwenye Ezekieli sura ya 1?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki