Matangazo
◼ Toleo la Juni: Kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? au Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Pia kitabu Ujuzi kinaweza kutolewa. Julai na Agosti: Yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 inaweza kutolewa: Endeleeni Kukesha!, Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Huenda broshua zifuatazo zikafaa sehemu fulani za eneo lenu: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli? na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? Septemba: Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kitatumiwa. Tutajitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia katika ziara ya kwanza. Ikiwa wenye nyumba tayari wana kitabu hicho, waonyeshe jinsi wanavyoweza kufaidika nacho kwa kuwaonyesha kwa ufupi jinsi funzo la Biblia linavyoongozwa.
◼ Mwangalizi-msimamizi au ndugu fulani aliyeteuliwa naye anapaswa kukagua hesabu za kutaniko za miezi ya Machi, Aprili, na Mei. Ukaguzi ukikamilishwa, kutaniko linapaswa kutangaziwa ripoti ya ukaguzi pamoja na ripoti ya hesabu itakayofuata.—Ona Maagizo ya Kufanyia Hesabu za Kutaniko (S-27).