Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Taarifa: Mkutano wa Utumishi wa kila juma utapangwa katika Huduma Yetu ya Ufalme wakati wa miezi ya kusanyiko la wilaya. Makutaniko yanaweza kufanya mabadiliko yanayohitajiwa ili kuhudhuria Kusanyiko la Wilaya la “Mfuateni Kristo!” Juma moja kabla ya kusanyiko tumieni dakika 15 katika Mkutano wa Utumishi ili kurudia mashauri na vikumbusho vinavyofaa hali zenu vilivyo katika nyongeza ya mwezi huu. Mwezi mmoja au miwili baada ya kusanyiko lenu, tumieni kati ya dakika 15 na 20 za Mkutano wa Utumishi (mnaweza kutumia sehemu ya mahitaji ya kwenu) kupitia mambo makuu ya kusanyiko ambayo yamewasaidia wahubiri katika huduma. Mwangalizi wa utumishi ashughulikie pitio hilo. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wanatumia au wanapanga kutumia habari hizo katika huduma yao.
Juma Linaloanza Juni 11
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Mei 15 na Amkeni! la Mei.
Dak. 15: Tumeandaliwa Kikamili Kuwa Walimu wa Neno la Mungu. Hotuba inayotegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi la Februari 15, 2002, ukurasa wa 24-28. Wakristo fulani husita kuanza kujifunza Biblia na watu wanaopendezwa kwa sababu wanajiona kuwa hawastahili kuongoza funzo. Hata hivyo, Yehova anatuwezesha kustahili kuwa wahudumu kupitia Neno lake, roho yake takatifu, na tengenezo lake. Kusudi letu si kuwaachia watu vichapo tu. Tunapaswa kujitahidi kuwafundisha watu. (Mt. 28:19, 20) Watie moyo wahubiri wajiwekee mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia.
Dak. 20: Fanyeni Mambo Yote kwa Utukufu wa Mungu. Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji yakitegemea sura ya 13 ya kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova.
Wimbo 144 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 18
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: Je, Unakumbuka? Mazungumzo na wasikilizaji yanayotegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 2007, ukurasa wa 19.
Dak. 20: “Tunafurahia Kutumiwa Kabisa Katika Utumishi wa Yehova!”a Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko ambayo hayakunukuliwa.
Wimbo 82 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Juni 25
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, onyesha jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Juni 1 na Amkeni! la Juni.
Dak. 20: “Tutaungana Ulimwenguni Pote Kutangaza Kusanyiko la Wilaya la ‘Mfuateni Kristo!’”b Mnapozungumzia fungu la 3, waalike wasikilizaji wasimulie mambo waliyojionea walipokuwa wakisambaza mialiko ya kusanyiko la wilaya la mwaka uliopita au utie ndani maelezo ya Kitabu cha Mwaka cha 2007, kuanzia ukurasa wa 7 hadi kichwa kidogo kwenye ukurasa wa 10.
Dak. 15: “Je, Unaweza Kuingia Kwenye ‘Mlango Mkubwa Unaoongoza Kwenye Utendaji’?”c Hoji kifupi painia mmoja au wawili wa kawaida. Walifanya marekebisho gani ili wafanye upainia wa kawaida? Wamepata baraka gani?
Wimbo 138 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Julai 2
Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Juni. Taja toleo la vichapo la Julai.
Dak. 10: “Endelea ‘Kuzaa Matunda Mengi.’”d Mnapozungumzia fungu la 4, tia ndani maelezo kuhusu sanduku “Jinsi ya ‘Kuzaa Matunda kwa Uvumilivu,’” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Februari 1, 2003, ukurasa wa 21.
Dak. 30: “Mfuateni Kristo kwa Kujiendesha kwa Heshima.”e Ishughulikiwe na mwandishi wa kutaniko. Taja kusanyiko ambalo kutaniko lenu limegawiwa. Pitia sanduku “Vikumbusho vya Kusanyiko la Wilaya.”
Wimbo 69 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
e Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.