Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Agosti 13
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Julai 15 na Amkeni! la Julai. Katika onyesho moja, mhubiri atumie mojawapo ya mapendekezo yaliyo katika fungu la 3, kwenye ukurasa wa 3 wa Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili 2007 kuuliza swali ambalo atajibu katika ziara ya kurudia. Zungumzia “Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko.” Tangaza tarehe za kusanyiko la mzunguko litakalofuata, ikiwa tarehe hizo zinajulikana.
Dak. 15: Faida za Kujitiisha kwa Mpango wa Kitheokrasi. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea sura ya 15 ya kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova.
Dak. 15: “Kumwabudu Yehova Tukiwa Familia.”a Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wamefaidika kwa kushiriki katika huduma wakiwa familia. Unaweza kupanga mapema ili mhubiri mmoja au wawili watoe maelezo kuhusu jambo hilo.
Wimbo 48 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 20
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Zungumzia “Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee,” na utangaze tarehe ya kusanyiko la pekee litakalofuata ikiwa inajulikana.
Dak. 15: Anzisha Funzo la Biblia Kwenye Ziara ya Kwanza Mwezi wa Septemba. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Mwezi wa Septemba tutatoa kitabu Biblia Inafundisha na kujitahidi kuzungumzia mafungu machache pamoja na mwenye nyumba kwenye ziara ya kwanza. Pitia mapendekezo yaliyo katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2006, na upange kuwe na onyesho moja au mawili ya jinsi ya kuanzisha funzo la Biblia kwenye ziara ya kwanza.
Dak. 20: “Jinsi Ambavyo Mpango wa Funzo la Kitabu la Kutaniko Hutusaidia.”b Mnapozungumzia fungu la 5, tia ndani maelezo kutoka kitabu Tengenezo, ukurasa wa 41, fungu la 2.
Wimbo 6 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 27
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Agosti 1 na Amkeni! la Agosti.
Dak. 10: “Jifanyieni Rafiki kwa Mali ya Udhalimu.” Hotuba itolewe na mzee kwa kutegemea Mnara wa Mlinzi la Desemba 1, 1994, ukurasa wa 13-18.
Dak. 25: “Mradi Mzuri kwa Ajili ya Mwaka Mpya wa Utumishi.”c Hoji mhubiri mmoja au wawili waliotumikia wakiwa mapainia-wasaidizi hivi karibuni. Walifanya marekebisho gani katika ratiba yao? Walifaidikaje? Ikiwezekana, mmoja wa wale wanaohojiwa anaweza kuwa mtu aliyefaulu kufanya upainia msaidizi kwa sababu ya kusaidiwa na kuungwa mkono na familia yao. Mnapozungumzia fungu la 9, taja tarehe za ziara itakayofuata ya mwangalizi wa mzunguko ikiwa zinajulikana.
Wimbo 196 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 3
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Habari za Kitheokrasi. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi za mwezi wa Agosti.
Dak. 15: “Tunathamini Mapendeleo Yetu!”d Wakati ukiruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yaliyoonyeshwa.
Dak. 20: Kikumbusho Muhimu na Sanduku la Swali.e
Wimbo 2 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
e Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.