Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/07 uku. 7
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma ya Ufalme—2007
Huduma ya Ufalme—2007
km 8/07 uku. 7

Matangazo

◼ Toleo la vichapo la Agosti: Broshua yoyote kati ya hizi zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutumiwa: Endeleeni Kukesha!, Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na“Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Katika sehemu fulani za eneo lenu, huenda ikafaa kutoa broshua zifuatazo: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? Septemba: Tutatoa kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitihada za pekee zinapaswa kufanywa ili kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza. Ikiwa tayari wenye nyumba wana kitabu hicho, waonyeshe jinsi wanavyoweza kufaidika na kitabu hicho kwa kuwaonyesha kwa ufupi jinsi ambavyo funzo la Biblia hufanywa. Oktoba: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Ikiwa upendezi unaonyeshwa, toa na uzungumzie trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? ukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia. Kitabu Ujuzi kinaweza kutolewa pia. Novemba: Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Mwenye nyumba akisema hana watoto, mtolee broshua Endeleeni Kukesha!

◼ Kwa kuwa mwezi wa Septemba una Jumamosi na Jumapili tano, utakuwa ni mwezi mzuri wa kufanya upainia msaidizi.

◼ Makutaniko yanapaswa kuanza kuagiza Kalenda ya Mashahidi wa Yehova ya Mwaka wa 2008, kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2008, na Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 2008 katika agizo lao la vitabu litakalofuata. Lugha ambazo vichapo hivyo vitapatikana itaonyeshwa katika barua ya kila mwezi ya vichapo.

◼ Wazee wanakumbushwa watekeleze maagizo yaliyo kwenye ukurasa wa 21-23 wa Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 1991, kuhusu watu waliotengwa au waliojitenga na ushirika ambao huenda wakataka kurudishwa.

◼ Sahihisho: Kwenye ukurasa wa 181, fungu la 2, katika kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, andiko la Wim. 3:39-42 limetajwa hapo kimakosa. Andiko linalopaswa kuwa hapo ni Omb. 3:39-42. Huenda ukapenda kuandika andiko hilo pambizoni mwa kitabu chako.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki