Pitio La Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatashughulikiwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Agosti 27, 2007. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Julai 2 hadi Agosti 27, 2007.
SIFA ZA USEMI
1. Tunaweza kuonyeshaje heshima kwa ajili ya wengine katika huduma yetu na katika kutaniko? [be uku. 192 fu. 2-4]
2. Ni mambo gani muhimu ili kuonyesha usadikisho tunapojieleza? [be uku. 196 fu. 1-3]
3. Ni mapendekezo gani yatakayotusaidia kuwa wenye busara tunapowatolea wengine ushahidi? [be uku. 198 fu. 1-5]
4. Tunapowatolea wengine ushahidi, kwa nini kujua wakati mzuri wa kutaja mambo ni muhimu? (Met. 25:11) [be uku. 199 fu. 1-3]
5. Tunaweza kuhakikishaje kwamba hotuba zetu ni zenye kutia moyo? [be uku. 203 fu. 3–uku. 204 fu. 1]
HOTUBA NA. 1
6. Ni jambo gani linaloweza kusemwa juu ya uandikaji wa Ezekieli, na pia juu ya kukubaliwa na uasilia wa kitabu cha Ezekieli? [si uku. 133 fu. 3]
7. Ili mtu avumilie kutotendewa haki anapaswa kuwa na sifa gani muhimu? [w05 6/1 uku. 29 fu. 4]
8. Tunajifunza nini kutokana na jibu la Yesu kwa Masadukayo ambao walimwuliza kuhusu ufufuo? (Luka 20:37, 38) [be uku. 66 fu. 4]
9. Mwanafunzi wa Biblia au mwamini mwenzetu anapouliza anapaswa kufanya nini chini ya hali fulani, unapaswa kujibuje? [be uku. 69 fu. 4-5]
10. Ni nini kinachohusika katika “kufanywa upya katika nguvu zinazoendesha akili”? (Efe. 4:23) [be uku. 74 fu. 4]
USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA
11. Katika Ezekieli 9:2-4, mwanamume aliyevaa kitani anawakilisha nani, na “alama kwenye mapaji ya uso” inamaanisha nini? [w88 9/15 uku. 14 fu. 18]
12. Viongozi wa kidini wa dini zinazodai kuwa za Kikristo wanafananaje na “manabii wajinga, wanaoifuata roho yao wenyewe,” wanaofafanuliwa katika Ezekieli 13:3? [w99 10/1 uku. 13]
13. Kwa kusema “neno . . . la kimethali” lililorekodiwa kwenye Ezekieli 18:2, Waisraeli walikuwa wakijaribu kufanya nini, na ni somo gani muhimu kuhusu kuwajibika linalokaziwa? [w88 9/15 uku. 18 fu. 10]
14. Ni katika maana gani Ezekieli alikuwa “bubu,” wakati wa kuzingirwa na kuharibiwa kwa Yerusalemu? (Eze. 24:27; 33:22) [w03 12/1 uku. 29]
15. “Gogu wa nchi ya Magogu” ni nani, naye anatenda lini ili kuangamiza watu wa Yehova? (Eze. 38:2, 16) [w97 3/1 uku. 14 fu. 1–uku. 15 fu. 3]