Kikumbusho Muhimu
‘Katika nchi kadhaa twasikia kuhusu “vyama” au vikundi vya watu wanaokusanya pesa kwa makusudi mbalimbali. Kwa kawaida wao hufanya mikutano au karamu katika nyumba mbalimbali kwa zamu, ambapo wote husaidia familia moja katika kikundi kwa “mkopo” au fedha za kulipia gharama kubwa sana. Ni kanuni gani za Biblia zinazoweza kuchunguzwa ili kuona msimamo wa Kikristo kuhusu jambo hili? Baadhi ya kanuni hizo ni Waefeso 5:3, 5 inayozungumza kuhusu pupa, Waroma 13:8 na Methali 22:7 kuhusu kukopa, 1 Wakorintho 15:33 na 2 Wakorintho 6:14, 15 kuhusu mashirika na mikataba na vilevile Waefeso 5:18 na 1 Petro 4:3 kuhusu kunywa au kufanya karamu na wasioamini. Kanuni hizo zinatosha na zinatuwezesha kufikia uamuzi unaofaa.’
Miaka kadhaa imepita tangu kikumbusho hiki kitolewe. Tangu wakati huo wengi wamekubali kweli. Kwa kuwa kuna hali ngumu za kiuchumi katika ulimwengu wa leo, wengi wetu watathamini kikumbusho hiki. Mshiriki wa kutaniko anapokuwa na uhitaji, ndugu mmoja-mmoja wanaweza kusaidia. Katika hali fulani, wazee wa kutaniko wanaweza kupanga kutoa msaada fulani.