Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/07 uku. 3
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma ya Ufalme—2007
Huduma ya Ufalme—2007
km 9/07 uku. 3

Matangazo

◼ Toleo la vichapo la Septemba: Tutatoa kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitihada za pekee zinapaswa kufanywa ili kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza. Ikiwa wenye nyumba wana kichapo hicho tayari, waonyeshe jinsi wanavyoweza kufaidika kwa kuwaonyesha jinsi ya kujifunza Biblia. Oktoba: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Ikiwa upendezi unaonyeshwa, toa na uzungumzie trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? ukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia. Kitabu Ujuzi kinaweza kutolewa pia. Novemba: Tutatoa kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Mwenye nyumba akisema hana watoto, mtolee broshua Endeleeni Kukesha! Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Pia unaweza kutoa kitabu Mkaribie Yehova au Siri ya Kupata Furaha ya Familia.

◼ Kwa kuwa mwezi wa Septemba una miisho-juma mitano, utakuwa mwezi mzuri wa kufanya upainia msaidizi.

◼ Makutaniko yanapaswa kuanza kuagiza mabuku ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ya 2007, Watch Tower Publications Index 2007, na Watchtower Library—2007 Edition katika CD-ROM kwenye agizo la vichapo litakalofuata. Makutaniko yatapokea orodha ya lugha ambazo vichapo hivyo vinapatikana kupitia “Barua kwa Makutaniko Yote,” ambayo hutumwa kila mwezi. Kumbukeni kwamba Watchtower Library—2007 Edition imetolewa kwa ajili ya ndugu na dada waliobatizwa na inaweza kuombwa tu kupitia kutaniko.

◼ Video Jehovah’s Witnesses—Organized to Share the Good News itazungumziwa katika Mkutano wa Utumishi mwezi wa Desemba. Ikihitajika, video hiyo inaweza kuagizwa kupitia kutaniko haraka iwezekanavyo.

◼ Hotuba ya pekee ya majira ya Ukumbusho ya mwaka wa 2008 itatolewa katika juma la Machi 31, 2008. Kichwa cha hotuba hiyo kitatangazwa baadaye. Makutaniko ambayo yatakuwa na ziara ya mwangalizi wa mzunguko au kusanyiko siku hiyo yatakuwa na hotuba hiyo juma linalofuata. Hotuba hiyo haipaswi kutolewa katika kutaniko lolote kabla ya juma la Machi 31, 2008.

◼ Mwangalizi-msimamizi au ndugu fulani aliyeteuliwa naye anapaswa kukagua hesabu ya kutaniko ya miezi ya Juni, Julai, na Agosti. Ukaguzi ukikamilishwa, kutaniko linapaswa kutangaziwa ripoti ya ukaguzi baada ya kusoma ripoti ya hesabu itakayofuata.—Ona Maagizo ya Kufanyia Hesabu za Kutaniko (S-27).

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki