Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
Juma Linaloanza Oktoba 8
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Septemba 15 na Amkeni! la Septemba. Katika kila onyesho magazeti yote mawili yatolewe hata kama ni moja tu litakalozungumziwa.
Dak. 20: Shikamana na Tengenezo la Yehova. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea sura ya 17 ya kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Juma Linaloanza Oktoba 15
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 20: Je, Kweli Inazaa Matunda Katika Wale Unaofundisha? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea Mnara wa Mlinzi la Februari 1, 2005, ukurasa wa 28-30. Tia ndani maelezo ya jinsi maswali katika kitabu Biblia Inafundisha yamekusudiwa kutambua kilicho moyoni mwa mwanafunzi. Fikiria mifano michache, sura ya 1, fungu la 19; sura ya 2, fungu la 4; sura ya 3, fungu la 24; na sura ya 4, fungu la 18. Watie moyo wahubiri watumie vizuri mambo mbalimbali yanayopatikana katika kitabu hicho.
Dak. 15: Je, Unakumbuka? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea Mnara wa Mlinzi la Agosti 15, 2007, ukurasa wa 19.
Juma Linaloanza Oktoba 22
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani kwa ajili ya michango. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1 na Amkeni! la Oktoba.
Dak. 15: “Tutatoa Toleo la Pekee la Amkeni! Mwezi wa Novemba!”a Kwa ufupi pitia yaliyomo katika Amkeni! la Novemba. Kisha zungumzia sehemu hii kwa maswali na majibu. Unapozungumzia fungu la 3, onyesha jinsi ya kutoa Amkeni! la Novemba ukitumia pendekezo lifuatalo: “Zamani watu walitafuta mwongozo katika Biblia. Lakini siku hizi wengi wana mashaka. Wewe una maoni gani? [Mruhusu ajibu. Kisha soma 2 Timotheo 3:16.] Toleo hili la pekee la Amkeni! linatoa uthibitisho wenye kusadikisha kwamba Biblia imeongozwa na roho ya Mungu.” Weka msingi kwa ajili ya ziara ya kurudia kabla ya kumaliza onyesho.
Dak. 20: Endeleeni Kutembea kama Wana wa Nuru. Hotuba na mahojiano. Tumeacha giza la ulimwengu huu na tumeruhusu tuongozwe na nuru ya Yehova. (Efe. 5:8, 9) Hilo limefanya maisha yetu yawe bora na yenye kusudi. (1 Tim. 4:8) Nuru hiyo pia inatupa tumaini. (Rom. 15:4) Wahoji wahubiri wawili au watatu ambao wamekabiliana na matatizo makubwa ili wapate na kudumisha uhusiano mzuri pamoja na Yehova na wakayashinda. Ni matatizo gani waliyopata walipokubali kweli? Waliwezaje kukabiliana nayo? Maisha yao ni bora sasa kwa njia gani? Ni nini kimewasaidia wawe imara katika kweli? Malizia kwa kuwatia moyo wote waendelee kufanya maendeleo ya kiroho na kuonyesha uthamini wa moyoni kwa kweli ambazo Yehova amefunua.—2 Pet. 1:5-8.
Juma Linaloanza Oktoba 29
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi za mwezi wa Oktoba. Taja toleo la mwezi wa Novemba na panga kuwe na onyesho moja la jinsi ya kulitoa.
Dak. 15: Jiwekee Miradi ya Kiroho Ili Kumtukuza Muumba Wako. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea Mnara wa Mlinzi la Julai 15, 2004, ukurasa wa 21-23. Waombe wasikilizaji wazungumzie miradi ya kiroho waliyojiwekea na kile ambacho wanafanya kuifikia. Unaweza kupanga mapema mtu mmoja au wawili wajitayarishe kutoa maelezo.
Dak. 20: “Wape Maskini Tumaini.”b Mnapochunguza fungu la 2 tia ndani maelezo kutoka Amkeni! la Septemba 8, 2003, ukurasa wa 26-27.
Juma Linaloanza Novemba 5
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: Jinsi ya Kuwalinda Watoto Wako Kupitia Hekima ya Mungu. Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Januari 1, 2005, ukurasa wa 23-27.
Dak. 20: “Ubadilishanaji wa Kitia-Moyo kwa Wote.”c Waombe wasikilizaji watoe maelezo hususa kuhusu jinsi walivyotiwa moyo na mwangalizi anayesafiri alipotembelea kutaniko. Unaweza kupanga mapema mtu mmoja au wawili wajitayarishe kutoa maelezo.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.