Matangazo
◼ Toleo la Februari: Kitabu Furaha ya Familia au kitabu Ujuzi. Machi: Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Tutajitahidi sana kuanzisha mafunzo ya Biblia. Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! na kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli. Jitahidi kuanzisha funzo la Biblia katika kitabu Mwabudu, hasa ikiwa watu fulani wamewahi kujifunza kitabu Biblia Inafundisha na broshua Anataka.
◼ Kwa kuwa mwezi wa Machi una miisho-juma mitano, utakuwa mwezi mzuri kufanya upainia msaidizi.
◼ Mwandishi na mwangalizi wa utumishi wanapaswa kupitia utendaji wa mapainia wote wa kawaida. Ikiwa kuna wowote wanaoshindwa kutimiza takwa la saa, wazee wanapaswa kupanga kuwasaidia.
◼ Hotuba ya pekee kwa ajili ya majira ya Ukumbusho ya mwaka wa 2008 itakuwa na kichwa “Ni Nani Anayestahili Kuwatawala Wanadamu?” Ona tangazo linalohusiana na hili kwenye Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 2007.