Matangazo
◼ Toleo la Machi: Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Tutajitahidi sana kuanzisha mafunzo ya Biblia. Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! na kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli. Jitahidi kuanzisha funzo la Biblia katika kitabu Mwabudu, hasa ukipata watu ambao wamewahi kujifunza kitabu Biblia Inafundisha na broshua Anataka. Juni: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia.
◼ Makutaniko yanapaswa kutoa magazeti mapya ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! mara tu yanapopokewa. Hilo litawasaidia wahubiri kufahamu yaliyomo kabla ya kuyatoa katika utumishi wa shambani.
◼ Mwangalizi-msimamizi au ndugu fulani aliyeteuliwa naye anapaswa kukagua hesabu za kutaniko za miezi ya Desemba, Januari, na Februari. Mtu yuleyule asitumiwe kufanya ukaguzi unaofuatana. Ukaguzi ukikamilishwa, kutaniko linapaswa kutangaziwa ripoti ya ukaguzi pamoja na ripoti ya hesabu itakayofuata.—Ona Maagizo ya Kufanyia Hesabu za Kutaniko (S-27).
◼ Kichwa cha makusanyiko ya wilaya ya 2008 ni “Kuongozwa na Roho ya Mungu.” Toleo la Juni la Huduma Yetu ya Ufalme litakuwa na habari yenye kina ya kuwasaidia kufanya mipango ya kibinafsi ili kuhudhuria sehemu zote za kusanyiko hili la siku tatu. Ikiwa unahitaji kuomba ruhusa kazini ili uhudhurie siku zote tatu, usisite kufanya hivyo.