Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/08 uku. 2
  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Aprili 14
  • Juma Linaloanza Aprili 21
  • Juma Linaloanza Aprili 28
  • Juma Linaloanza Mei 5
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 4/08 uku. 2

Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Juma Linaloanza Aprili 14

Wimbo 183

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 6 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Machi 1 na Amkeni! la Machi.

Dak. 15: “Mjionyeshe Kuwa Wenye Shukrani.”a Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko ambayo hayakunukuliwa.

Dak. 20: “Wafariji Wale Wanaoomboleza.”b Waombe wasikilizaji wasimulie jinsi ambavyo wamemfariji mtu aliyempoteza mpendwa katika kifo.

Wimbo 42

Juma Linaloanza Aprili 21

Wimbo 171

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani. Wakumbushe wasikilizaji waje na Mnara wa Mlinzi la Aprili 1 na Amkeni! la Aprili kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma lijalo na wajitayarishe kuzungumzia njia zinazofaa za kutoa magazeti hayo katika eneo lenu.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: Mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi akazia mambo makuu katika sura ya 8 ya kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kuhusu kiasi kinachofaa cha sauti. Watie moyo wote watoe maelezo kwa sauti kubwa katika mkutano wa Funzo la Kitabu la Kutaniko ili wote wafaidike.

Wimbo 197

Juma Linaloanza Aprili 28

Wimbo 55

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Aprili. Eleza kwa ufupi yaliyomo katika Mnara wa Mlinzi la Aprili 1 na Amkeni! la Aprili kisha uwaombe wasikilizaji wataje makala ambazo huenda zikawapendeza watu katika eneo na kwa nini. Waombe wasikilizaji wataje mambo wanayopanga kusema shambani wanapokazia makala hizo. Wanaweza kuuliza swali gani ili kuanzisha mazungumzo? Kisha wanaweza kusoma andiko gani linalopatikana katika makala hiyo? Andiko hilo linaweza kuhusianishwaje na swali ambalo waliuliza? Ukitumia pendekezo moja la wasikilizaji au mapendekezo mengine katika Huduma Yetu ya Ufalme, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa kila moja ya magazeti hayo.

Dak. 10: Sanduku la Swali. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji.

Dak. 20: “Fuata Hatua Zake kwa Ukaribu.”c Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko ambayo hayakunukuliwa.

Wimbo 65

Juma Linaloanza Mei 5

Wimbo 217

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.

Dak. 15: Yehova Hatakuacha Hata Kidogo. Hotuba yenye kutia moyo inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Oktoba 15, 2005, ukurasa wa 8-11.

Dak. 20: “Fanya Maendeleo Katika Kazi ya Kuhubiri.”d Mnapozungumzia fungu la 3, tia ndani maelezo kutoka katika kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 6-8, chini ya kichwa kidogo “Jinsi ya Kufaidika Kabisa.”

Wimbo 11

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki