Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
Juma Linaloanza Mei 12
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Aprili 1 na Amkeni! la Aprili.
Dak. 15: Tunaweza Kuvumilia Jaribu Lolote Lile! Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 2005, ukurasa wa 30-31. Waombe wahubiri uliowateua wasimulie jinsi ambavyo Yehova aliwasaidia kukabili jaribu fulani.
Dak. 20: Je, Unaweza Kufanya Upainia Msaidizi Wakati wa Likizo? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Pitia habari zilizo katika kitabu Tengenezo ukurasa wa 112-113, na utaje matakwa ya kujiandikisha. Waalike wale ambao wamefanya upainia msaidizi baada ya kuchukua likizo kazini waeleze baraka ambazo wamepata. Waombe wale ambao wamefanya upainia msaidizi wakati wa likizo ya shule waeleze jinsi ambavyo wengine waliwatia moyo na kuwasaidia. Upainia msaidizi uliwasaidiaje kufanya maendeleo ya kiroho? Walipata shangwe gani? Watie moyo wote wanaostahili wafikirie kufanya upainia wakati wa likizo.
Juma Linaloanza Mei 19
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia Sanduku la Swali.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: “Unaweza Kupata Utajiri!”a Eleza matakwa ya kuwa painia wa kawaida, yaliyo katika kitabu Tengenezo ukurasa wa 113-114. Wale ambao wangependa kuanza upainia Septemba 1 wanapaswa kutoa maombi yao haraka iwezekanavyo.
Juma Linaloanza Mei 26
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Mei. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa Mnara wa Mlinzi la Mei 1 na Amkeni! la Mei.
Dak. 15: “Chukueni Nira Yangu.”b Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko ambayo hayakunukuliwa.
Dak. 20: Tumia kitabu Biblia Inafundisha mwezi wa Juni. Hotuba na maonyesho. Pitia baadhi ya njia za kuhubiri zinazoonyeshwa katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2006. Tia ndani onyesho lenye sehemu mbili. Onyesha jinsi kitabu hicho kinavyoweza kutolewa na jinsi ya kufanya ziara ya kurudia ili kuanzisha funzo la Biblia.
Juma Linaloanza Juni 2
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 20: Watu Wenye Matendo ya Uaminifu Wanapata Baraka Nyingi. (Met. 28:20) Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakiongozwa na mwandishi. Onyesha jinsi ambavyo Yehova amebariki jitihada za kutaniko za kuongeza utumishi mwezi wa Machi, Aprili, na Mei, na utoe pongezi. Tangaza idadi ya wale waliofanya upainia msaidizi, mafunzo mapya ya Biblia yaliyoanzishwa, na mambo mengine mazuri yaliyotimizwa katika huduma. Waombe wasikilizaji wasimulie mambo yaliyoonwa kuhusiana na Ukumbusho na kampeni ya kugawa mialiko. Mambo yenye kupendeza kuhusu utumishi wa shambani yanaweza kuigizwa. Wahoji kwa ufupi wahubiri wawili au watatu kuhusu baraka ambazo walipata wakiwa mapainia-wasaidizi.
Dak. 15: “Uwe Tayari kwa Ajili ya Kila Kazi Njema.”c Waombe wasikilizaji waeleze jinsi wanavyojitayarisha kwa ajili ya huduma ya nyumba kwa nyumba na wakati ambapo wanafanya hivyo.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.