Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Juni 30, 2008. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Mei 5 hadi Juni 30, 2008. [Taarifa: Mahali ambapo vichapo vya marejeo havijaonyeshwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]
SIFA ZA USEMI
1. Tunaweza kufanya nini ili kuhakikisha kwamba mifano tunayotumia inaeleweka? [be uku. 242 fu. 3–uku. 243 fu. 1]
2. Kwa nini mifano rahisi inayohusu hali za kawaida inafaa? [be uku. 245 fu. 2-4]
3. Kutumia vielelezo vizuri ni muhimu kadiri gani, na Yehova alivitumiaje kufundisha masomo muhimu? (Mwa. 15:5; Yer. 18:6; Yona 4:10, 11) [be uku. 247 fu. 1-2]
4. Ni jinsi gani tunaweza kutumia vielelezo kuboresha ufundishaji wetu? [be uku. 248 fu. 1-3]
5. Tunaweza kutumiaje ramani kama vielelezo vinavyofaa kuwafundisha wanafunzi wa Biblia? [be uku. 248 fu. 4]
HOTUBA NA. 1
6. Kwa msaada wa roho takatifu ya Mungu, kujifunza Biblia kutatusaidia kufahamu nini? [be uku. 32 fu. 2-3]
7. Tunaweza kutumiaje Biblia yenyewe kufanya utafiti ili kupata maana ya andiko fulani? [be uku. 34 fu. 4–uku. 35 fu. 2]
8. Fungu la Yesu akiwa kipitio pekee ambacho kwacho baraka za Yehova zawafikia ainabinadamu limekaziwaje katika Injili ya Yohana? [si uku. 198 fu. 32]
9. Kuna msingi gani wa Kimaandiko wa kwamba tabibu Luka ndiye aliyeandika kitabu cha Matendo? [si uku. 199 fu. 3; uku. 200 fu. 5-7]
10. Kwa kawaida, mtu anapaswa kufuata hatua gani anapotayarisha muhtasari wa hotuba? [be uku. 39-41]
USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA
11. Ni hekalu gani ambalo “lilijengwa kwa miaka 46”? (Yoh. 2:20) [w08 4/15 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yohana”]
12. Ni nani ambao ‘wamevuka kutoka katika kifo na kuingia katika uzima’? (Yoh. 5:24, 25) [w08 4/15 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yohana”]
13. Ni kwa njia gani Yesu ‘angetayarisha mahali’ mbinguni kwa ajili ya wafuasi wake waaminifu? (Yoh. 14:2) [w08 4/15 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yohana”]
14. Kwa nini Yesu alimwambia Maria Magdalene aache kumng’ang’ania? (Yoh. 20:17) [w08 4/15 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yohana”]
15. Biblia inamaanisha nini inaposema kwamba Yesu atakuja “vivyo hivyo” kama alivyopanda mbinguni? (Mdo. 1:9-11) [rs uku. 117 fu. 4; it-1 uku. 186 fu. 8]