Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/08 uku. 5
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 6/08 uku. 5

Matangazo

◼ Toleo la mwezi wa Juni: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Fanyeni jitihada za pekee za kuanzisha mafunzo ya Biblia. Julai na Agosti: Tumia broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32: Endeleeni Kukesha!, Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na broshua “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! na broshua nyingine zinazopatikana katika lugha nyinginezo. Septemba: Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kitatumiwa. Fanya jitihada za pekee kuanzisha funzo la Biblia kwenye ziara ya kwanza. Ikiwa tayari wenye nyumba wana kitabu hicho, onyesha jinsi wanavyoweza kufaidika kutokana nacho kwa kuwaonyesha kwa ufupi jinsi funzo la Biblia linavyoongozwa.

◼ Kwa kuwa mwezi wa Agosti una Jumamosi tano na Jumapili tano, utakuwa mwezi mzuri wa kufanya upainia msaidizi.

◼ Mtu fulani aliyeteuliwa na mwangalizi-msimamizi anapaswa kukagua hesabu za kutaniko za miezi ya Machi, Aprili, na Mei. Ukaguzi ukikamilishwa, kutaniko linapaswa kutangaziwa baada ya ripoti ya hesabu itakayofuata kusomwa.—Ona Maagizo ya Kufanyia Hesabu za Kutaniko (S-27).

◼ Inapendekezwa kwamba maombi ya kuwa painia wa kawaida yatumwe kwenye ofisi ya tawi angalau siku 30 kabla ya tarehe ya kuanza iliyoombwa. Mwandishi wa kutaniko anapaswa kupitia fomu hizo kuhakikisha kwamba zimejazwa vizuri. Kama waombaji hawakumbuki tarehe hususa ambayo walibatizwa, wanaweza kukadiria tarehe na kuweka kumbukumbu. Mwandishi anapaswa kuandika tarehe hiyo kwenye kadi ya Rekodi ya Kutaniko ya Mhubiri (S-21).

◼ Kuanzia Januari 2008, magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yaliyorekodiwa katika Kiingereza yamewekwa kwenye kituo cha Intaneti cha www.jw.org. Wengi wanapendelea kupata magazeti hayo yaliyorekodiwa kutoka kwenye kituo hicho kwa kuwa yanapatikana kabla ya CD za kawaida au za MP3 kufika katika makutaniko. Kila mara mtu anapochukua magazeti kwenye kituo hicho, tengenezo linalipa kiasi fulani cha pesa. Hata hivyo, kusambaza magazeti kwa njia hiyo hakugharimu pesa nyingi kama kutengeneza na kusafirisha CD. Kwa hivyo, wahubiri wanaochukua magazeti yaliyorekodiwa kwenye kituo hicho wanahimizwa wamfikie mtumishi wa magazeti na kufuta maagizo yao ya CD au MP3. Magazeti ya lugha nyingine yatapatikana kwenye kituo cha www.jw.org. hatua kwa hatua.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki