Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
Juma Linaloanza Julai 14
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 1 na Amkeni! la Juni.
Dak. 15: Je, Wewe Una “Uhuru wa Kusema”? Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Mei 15, 2006, ukurasa wa 13-16. Kazia umuhimu wa kuhubiri kwa ujasiri.
Dak. 20: “Izingatie Siku ya Yehova Maishani.”a Taja mambo ya pekee katika kitabu hicho. Pitia ratiba ya funzo la kitabu na maagizo yaliyo katika ukurasa wa 3 wa toleo hili la Huduma Yetu ya Ufalme. Watie moyo wote wahudhurie kwa ukawaida na watoe maelezo kwa uhuru. Mhoji kwa ufupi mhubiri mmoja au wawili ambao wanajulikana kwa kujitayarisha vizuri kwa ajili ya mikutano, na uwaulize kinachowachochea kufanya hivyo.
Juma Linaloanza Julai 21
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Wakumbushe wasikilizaji waje na gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 1 na Amkeni! la Julai kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma lijalo na wajitayarishe kuzungumzia njia zinazofaa wanazopanga kutumia kutoa magazeti hayo.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: “Kujitayarisha—Siri ya Kufanya Ziara za Kurudia Zenye Manufaa.”b Tia ndani onyesho la dakika nne la mhubiri anayejizungumzia anapojitayarisha kwa ajili ya ziara za kurudia. Anapitia rekodi zake na kutambua kwamba anahitaji kuwarudia watu wawili mwishoni mwa juma hili. Kisha, anajikumbusha mambo aliyozungumzia pamoja na kila mmoja wa watu hao, anatambua lengo lake, na kutayarisha jinsi atakavyofikia lengo hilo. Anajiandaa kuanzisha funzo la Biblia pamoja na yule mtu wa kwanza. Pia, akitumia pendekezo fulani katika fungu la 5, anajitayarisha kumchochea yule mtu wa pili apendezwe zaidi.
Juma Linaloanza Julai 28
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote watoe ripoti za utumishi wa shambani za Julai. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani. Taja toleo la Agosti, na upange kuwe na onyesho moja.
Dak. 15: Kudumisha Mtazamo Wetu wa Uharaka. Hotuba yenye kuchochea inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Desemba 15, 2006, ukurasa wa 18-19, fungu la 17-21.
Dak. 20: Jitayarishe Kutoa Magazeti ya Karibuni. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Baada ya kuzungumzia kwa ufupi mambo makuu katika gazeti la Amkeni! la Julai na Mnara wa Mlinzi la Julai 1, waombe wasikilizaji waeleze makala ambazo zinaweza kuwavutia watu katika eneo lenu na kwa nini. Waombe wataje mambo hususa ambayo wanapanga kuwaonyesha watu katika makala hizo. Ni swali gani linaloweza kuulizwa ili kuanzisha mazungumzo? Kisha, ni andiko gani katika makala linaloweza kusomwa? Ukitumia pendekezo moja kati ya mapendekezo yaliyo katika Huduma Yetu ya Ufalme au pendekezo lingine la wasikilizaji, panga onyesho la jinsi ya kutoa kila moja ya magazeti hayo.
Juma Linaloanza Agosti 4
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: Je, Watoto Wako Wako Tayari Kuhubiri Katika Eneo Lao la Pekee? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Taja matatizo fulani ambayo vijana Wakristo hukabili shuleni. Eleza jinsi wazazi na watoto wao wanavyoweza kutumia Fahirisi kupata habari zitakazowasaidia. Toa mifano kadhaa. (Ona kichwa kikuu “Shule,” kisha habari yenye kichwa “mambo yaliyoonwa.”) Waombe wasikilizaji waliolelewa katika familia za Kikristo waeleze jinsi wazazi wao walivyowatayarisha kukabili matatizo na kutumia kanuni za Biblia shuleni. Wanaweza kutaja pia migawo ya shule waliyotayarisha wakitumia habari zilizo katika Amkeni! Waombe waeleze jinsi ambavyo kuhubiri katika eneo lao la pekee kuliwalinda.
Dak. 20: “Tunapindua Ngome Zenye Nguvu.”c Waombe wasikilizaji waeleze jinsi mwalimu wao wa Biblia alivyowasaidia kwa subira kuacha mafundisho ya uwongo ya kidini ambayo waliyashikilia sana.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.