Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/08 uku. 3
  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 8/08 uku. 3

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Agosti 25, 2008. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Julai 7 hadi Agosti 25, 2008.

SIFA ZA USEMI

1. Tunawezaje kuonyesha tunakubali sababu tunaposhiriki kweli na wengine? (Flp. 4:5) [be uku. 251 fu. 3]

2. Mfano wa Paulo alipozungumza na Wagiriki katika Areopago utatusaidiaje tunapowahubiria wale ambao hawaoni umuhimu wa Biblia? (Mdo. 17:22, 23) [be uku. 252 fu. 1-2]

3. Hata ikiwa tuna hakika ya kwamba mtu tunayezungumza naye amekosea, tunaweza kuonyeshaje tunakubali sababu tunaposhughulika naye? [be uku. 253 fu. 1-2]

4. Tunapojaribu kuzungumza kwa usadikisho, tunapaswa kukumbuka nini? [be uku. 255 fu. 3, sanduku]

5. Tunaweza kutumiaje utambuzi tunapojitahidi kufikia moyo wa msikilizaji? (Met. 20:5) [be uku. 258 fu. 1-5]

HOTUBA NA. 1

6. Akina dada wanapaswa kukumbuka nini wanapopata mgawo unaohusu kikao? [be uku. 44 fu. 5-6]

7. Akina ndugu wanapaswa kujitahidi kutimiza nini wanapotoa mambo makuu ya usomaji wa Biblia? (Neh. 8:8) [be uku. 47 fu. 2-3]

8. Ndugu anapaswa kutunzaje mgawo katika Mkutano wa Utumishi ulio na maonyesho au mahojiano? [be uku. 49 fu. 5]

9. Kitabu cha Matendo kinaonyeshaje ni kwa njia na kwa kadiri gani ushahidi utatolewa? (Mdo. 20:20, 21; 28:23) [si uku. 204 fu. 35]

10. Msemaji anaweza kufanya nini ili kuhakikisha kwamba Biblia ni msingi wa hotuba yake? (Mdo. 17:2, 3) [be uku. 52 fu. 6–uku. 53 fu. 2]

USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA

11. Kwa nini mlinzi Mfilipi wa jela alitaka “kujiua”? (Mdo. 16:25-27) [w90 5/15 uku. 25, sanduku]

12. Aristarko na Gayo walifanya nini walipoteswa? (Mdo. 19:29; 20:4, 5) [w08 2/15 uku. 10 fu. 16-17]

13. Ilimaanisha nini kwamba Sauli alikuwa ‘akiipiga teke michokoo’? (Mdo. 26:14) [w03 10/1 uku. 32]

14. Ni jinsi gani ‘dhambi ilichochewa’ kupitia amri ya Mungu kwa Waisraeli? (Rom. 7:8, 11) [w08 6/15 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Barua kwa Waroma”]

15. Tunakusanya “makaa yenye moto” juu ya kichwa cha adui jinsi gani? (Rom. 12:20) [w08 6/15 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Barua kwa Waroma”]

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki