Matangazo
◼ Toleo la Agosti: Tumia broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32: Endeleeni Kukesha!, Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote? Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, Serikali Itakayoleta Paradiso, “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! na broshua nyingine zinazopatikana katika lugha nyinginezo. Septemba: Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kitatumiwa. Jitahidi sana kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza. Ikiwa tayari wenye nyumba wana kitabu hiki, waeleze jinsi wanavyoweza kufaidika kwa kuwaonyesha kwa ufupi jinsi wanavyoweza kujifunza Biblia. Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Ikiwa mtu anapendezwa, mwonyeshe trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? na uizungumzie ukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia. Novemba: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi sana kuanzisha mafunzo ya Biblia. Unaweza pia kuwaachia watu kitabu Ujuzi ili wajisomee.
◼ Makutaniko yanapaswa kuanza kuagiza Kalenda ya 2009 ya Mashahidi wa Yehova, Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2009, na Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 2009 katika ombi linalofuata la vitabu. Orodha ya lugha ambazo vifaa hivyo vitapatikana itachapishwa katika barua yenye kichwa “Tangazo kwa Makutaniko Yote,” inayotumwa kila mwezi kwa makutaniko yote.
◼ Wazee wanakumbushwa watekeleze maagizo yaliyo kwenye ukurasa wa 21-23 wa Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 1991, kuhusu watu waliotengwa au waliojitenga na ushirika ambao huenda wangependa kurudishwa kutanikoni.
◼ Ili kuwasaidia wahubiri na watu wanaopendezwa ambao ni vipofu na wenye matatizo ya kuona ambao wanatumia vifaa vinavyoandika maandishi ya vipofu au kompyuta zinazosoma maandishi kwa sauti, mpango umefanywa wa kuwaandalia faili za elektroniki za maandishi ya vipofu za Mnara wa Mlinzi. Faili hizo zinatia ndani toleo la watu wote na toleo la funzo la Mnara wa Mlinzi Gredi ya 2, au maandishi ya vipofu ya Kiingereza yaliyofupishwa na matoleo ya funzo ya Mnara wa Mlinzi ya Gredi ya 1, au maandishi ya Kifaransa ambayo hayajafupishwa. Faili hizo zitatumwa kupitia barua-pepe kwa wale wanaoziagiza. Wale ambao wangependa kupokea faili za Mnara wa Mlinzi za maandishi ya vipofu wanapaswa kumwomba mwandishi wa kutaniko aandike barua na kuituma kwenye ofisi ya tawi au ofisi inayosimamia kazi nchini. Barua hiyo inapaswa kuonyesha jina la mtu huyo, anwani yake, jina au aina ya kifaa cha elektroniki anachotumia, anwani yake ya barua-pepe, na iwapo anasoma maandishi ya vipofu ya Kiingereza au ya Kifaransa. Ikiwa hana anwani ya barua-pepe, anapaswa kutumia anwani ya barua-pepe ya mtu mwingine ambaye anaweza kupokea faili hizo na kumtumia.