Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
Juma Linaloanza Agosti 11
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu makala za magazeti ya karibuni ambazo wameona zinawavutia watu katika eneo lenu. Waombe wataje mambo hususa katika makala hizo ambayo wanapanga kuwaonyesha watu. Wanaweza kuuliza swali gani ili kuanzisha mazungumzo? Ni andiko gani katika makala hizo ambalo wanaweza kusoma? Panga maonyesho yanayoonyesha jinsi mapendekezo hayo yanavyoweza kutumiwa.
Dak. 15: Fanya Mapenzi ya Mungu—Bila Kukengeushwa. Hotuba inayotegemea kitabu ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu,’ ukurasa wa 93-94, fungu la 12-13.
Dak. 20: “Je, Unalitumia Kikamili?”a Mhoji mhubiri ambaye alipata matokeo alipotumia moja ya makala mpya za toleo la watu wote la Mnara wa Mlinzi. Jambo hilo lililoonwa linaweza kuigizwa. Pia, ukitumia fungu la 2, panga onyesho linaloonyesha jinsi funzo linavyoweza kuanzishwa kwa kutumia makala yenye kichwa “Tunayojifunza Kutoka kwa Yesu,” katika Mnara wa Mlinzi la Agosti 1 au toleo la karibuni zaidi.
Juma Linaloanza Agosti 18
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Zungumzia “Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko.” Tangaza tarehe ya kusanyiko linalofuata la mzunguko ikiwa inajulikana. Wakumbushe wasikilizaji waje na gazeti la Mnara wa Mlinzi la Agosti 1 na Amkeni! la Agosti kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma lijalo na wawe tayari kueleza jinsi magazeti hayo yanavyoweza kutumiwa katika eneo lenu.
Dak. 20: Mavazi na Mapambo Yetu Yanamletea Yehova Heshima. Hotuba itolewe na mzee. Kwa sababu Yehova ni Mungu mtakatifu, ni muhimu sana watu wake wawe safi kimwili. (Kut. 30:17-21; 40:30-32) Tunampendeza Yehova na kumletea utukufu tunapovalia na kujipamba kwa njia nzuri, hasa katika huduma yetu. (1 Pet. 2:12) Hata hivyo, tukivaa na kujipamba kwa njia isiyofaa, tunafanya ‘neno la Mungu litukanwe.’ (Tito 2:5) Simulia mambo yaliyoonwa ya kwenu au yaliyochapishwa ambayo yanaonyesha jinsi mhubiri alivyotoa ushahidi mzuri kwa sababu ya kuvalia vizuri.
Dak. 15: Vijana Wanaotoa Ushahidi Mzuri Sana. Hotuba ya kuwatia moyo wazazi na watoto wao ambao wanajitayarisha kurudi shuleni. Wakumbushe vijana watumie nafasi wanazopata kuhubiri. Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji wasimulie jinsi walivyotoa ushahidi shuleni.
Juma Linaloanza Agosti 25
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani. Zungumzia “Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee,” na utangaze tarehe ya kusanyiko la pekee linalofuata ikiwa inajulikana.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 15: Jitayarishe Kutoa Mnara wa Mlinzi la Agosti 1 na Amkeni! la Agosti. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Zungumzia kwa ufupi magazeti hayo na uwaombe wasikilizaji wataje makala ambazo zinaweza kuwavutia watu katika eneo lenu na swali na andiko ambalo wanaweza kutumia kuanzisha mazungumzo. Panga mhubiri aonyeshe jinsi utangulizi unaopendekezwa kwenye Huduma Yetu ya Ufalme unavyoweza kutumiwa. Panga mzee mmoja afanye onyesho fupi ambalo ametayarisha akitumia makala ambayo itafaa eneo lenu.
Juma Linaloanza Septemba 1
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Agosti. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 20: Wako Peke Yao Lakini Hawajasahauliwa. Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Aprili 15, 2008, ukurasa wa 25-28. Wataje Wakristo wa kutaniko lenu ambao wanaishi katika makao ya kuwatunzia wazee. Ikiwa hakuna yeyote, tumia kanuni zilizo katika makala hiyo kulitia moyo kutaniko limtegemeze Shahidi yeyote ambaye hawezi kushiriki sana katika utendaji wa kutaniko kwa sababu ya ugonjwa au ulemavu.
Dak. 15: Anzisha Funzo la Biblia Katika Ziara ya Kwanza Mwezi wa Septemba. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Katika mwezi wa Septemba tutatumia kitabu Biblia Inafundisha katika utumishi na kujitahidi kuzungumzia mafungu machache pamoja na wenye nyumba katika ziara ya kwanza. Zungumzia kwa ufupi mapendekezo yaliyo katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2006 na upange onyesho moja au mawili kuhusu kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.