Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
Juma Linaloanza Septemba 8
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Waombe wasikilizaji waeleze makala za magazeti ya karibuni ambazo zinaweza kuwavutia watu zaidi katika eneo lenu. Waombe wataje maswali na maandiko ambayo wametumia wanapozungumzia makala hizo. Panga maonyesho yatakayoonyesha jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa.
Dak. 15: Wasaidie Wanafunzi wa Biblia Wawe Walimu. Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 2007, ukurasa wa 29-30, fungu la 14-20. Tia ndani onyesho fupi linaloonyesha mhubiri akimweleza mwanafunzi mpya wa Biblia kuhusu hotuba ya watu wote na Funzo la Mnara wa Mlinzi, kisha anamwalika ahudhurie.
Dak. 20: Kukabiliana na Ubaguzi Katika Huduma Yetu. Hotuba itolewe na mzee, ikitegemea habari iliyochapishwa inayoonyesha jinsi ubaguzi unavyoweza kuathiri huduma yetu. Eleza jinsi tunavyoweza kushinda ubaguzi huo. Nyakati nyingine, mwenendo wetu katika huduma ya shambani na katika shughuli nyingine za maisha unaweza kuthibitisha kwamba maoni ya watu wenye ubaguzi hayana msingi na unaweza kuwachochea wakubali kweli. Kwa hiyo, nyakati zote tunapaswa kuwa waangalifu kuhusu yale tunayosema na kutenda. (1 Pet. 2:12; 3:1, 2) Simulia mambo machache yaliyoonwa na wahubiri wa kwenu au mambo yaliyoonwa yaliyochapishwa yanayoonyesha jinsi tunavyoweza kushinda ubaguzi.
Juma Linaloanza Septemba 15
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 20: Tulitimiza Nini Mwaka Uliopita? Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakiongozwa na mwangalizi wa utumishi au mzee mwingine anayestahili. Zungumzia utendaji wa kutaniko katika huduma katika mwaka uliopita wa utumishi, ukikazia mambo mazuri yaliyotimizwa. Toa pongezi kwa mambo mazuri yaliyotimizwa. Panga mapema ili mhubiri mmoja au wawili wasimulie mambo yoyote ya pekee ambayo walipata katika huduma. Taja jambo moja au mawili ambayo kutaniko linaweza kuboresha katika mwaka unaokuja, na utoe mapendekezo yatakayowasaidia kufanya maendeleo.
Dak. 15: Ninaweza Kuteteaje Imani Yangu Kuhusu Uumbaji? Hotuba inayotegemea habari zilizochapishwa. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wametetea imani yao kuhusu uumbaji wakiwa shuleni, kazini, au mahali pengine. Unaweza kupanga ili mmoja au wawili wajitayarishe mapema kutoa maelezo.
Juma Linaloanza Septemba 22
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani. Zungumzia barua kutoka kwa ofisi ya tawi iliyo kwenye ukurasa wa 1.
Dak. 20: Utapata Thawabu kwa Kazi Yako. Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi, Aprili 15, 2005, kuanzia ukurasa wa 28, fungu la 6, mpaka mwisho wa ukurasa wa 29. Muulize mhubiri mmoja au wawili wenye bidii waeleze kwa ufupi jinsi Yehova alivyotimiza mahitaji yao ya kimwili na kuwategemeza kihisia.
Dak. 15: Jitayarishe Kutoa Mnara wa Mlinzi la Septemba 1 na Amkeni! la Septemba. Zungumzia magazeti hayo kwa ufupi, kisha uwaombe wasikilizaji waeleze makala ambazo zinaweza kuwavutia watu katika eneo lenu. Ni maswali na maandiko gani ambayo wanaweza kutumia wanapozungumzia makala hizo? Panga mhubiri aonyeshe jinsi pendekezo lililo katika Huduma Yetu ya Ufalme linavyoweza kutumiwa. Panga mzee mmoja atoe onyesho fupi akitumia makala ambayo itafaa eneo lenu.
Juma Linaloanza Septemba 29
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti za utumishi wa shambani za Septemba. Panga mapema ili mhubiri mmoja au wawili wasimulie mambo yaliyoonwa yenye kujenga waliyopata walipokuwa wakihubiri isivyo rasmi wakati wa kusanyiko la wilaya, likizo, au katika pindi nyingine.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: “Kampeni ya Pekee ya Trakti Kuanzia Oktoba 20 Hadi Novemba 16!”a Ikiwa trakti zipo, mpe kila msikilizaji trakti moja. Unapozungumzia fungu la 2, eleza kwa ufupi mambo yaliyo katika trakti hiyo. Unapozungumzia fungu la 4, panga onyesho la kutoa trakti hiyo. Unapozungumzia fungu la 5, panga onyesho la mhubiri akitumia trakti hiyo kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kurudia.
Juma Linaloanza Oktoba 6
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.
Dak. 15: Sanduku la Swali. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tia ndani maelezo kutoka katika Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 2005, ukurasa wa 20-22, fungu la 10-16.
Dak. 20: “Wafundishe Wengine Kumpenda Yehova.”b Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko ambayo hayakunukuliwa.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.