Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Oktoba 27, 2008. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Septemba 1 hadi Oktoba 27, 2008.
SIFA ZA USEMI
1. Tunaweza kufanya nini ili tujue kwa nini watu wana maoni fulani? [be uku. 259 fu. 1, 2]
2. Tunaweza kumsaidiaje mtu aondoe chuki au ubaguzi moyoni mwake? [be uku. 260 fu. 2]
3. Tunaweza kuwasaidiaje wanafunzi wetu wajichunguze moyoni ili waendelee kukua kiroho? [be uku. 261 fu. 2]
4. Tunapaswa kukumbuka nini tunapojitahidi kuugusa moyo wa wasikilizaji wetu? [be uku. 262 fu. 4]
5. Kwa nini tunapaswa kufuata wakati katika mikutano ya kutaniko? [be uku. 263 fu. 1, 3, sanduku]
HOTUBA NA. 1
6. Ni nini kilichomsukuma Paulo kuandika barua yake ya kwanza kwa Wakorintho? [si uku. 210 fu. 3]
7. Ni baadhi ya mambo gani yaliyomfanya Paulo aandike barua yake ya pili kwa Wakorintho? [si uku. 214 fu. 1-2]
8. Wakristo wanapaswa kuionaje huduma? [si uku. 216-217 fu. 18]
9. Kama vile ndugu Wafilipi, tunawezaje leo kupata kibali cha Mungu na kuwa shangwe kwa ndugu zetu? [si uku. 225 fu. 12]
10. Paulo na wahudumu wenzake waliweka kielelezo gani bora kwa kutaniko la Thesalonike? [si uku. 231 fu. 13]
USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA
11. Ni nini maana ya maneno, “mkamkabidhi mtu [mwovu] kwa Shetani kwa ajili ya kuangamizwa kwa mwili, ili roho iokolewe”? (1 Kor. 5:5) [w08 7/15 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Barua kwa Wakorintho”]
12. Ni kwa njia gani kifo cha Yesu kinapaswa kuadhimishwa “kila mara,” nacho kinapaswa kuadhimishwa “mpaka” wakati gani? (1 Kor. 11:26) [w08 7/15 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Barua kwa Wakorintho”]
13. Ni maono gani yanayotajwa katika 2 Wakorintho 12:2-4, na inaelekea ni nani aliyeona maono hayo? [w04 10/15 uku. 8 fu. 4; uku. 10 fu. 9]
14. Kwa nini Paulo alilinganisha Sheria ya Musa na ‘mtunzaji anayeongoza kwa Kristo’? (Gal. 3:24) [w08 3/1 uku. 18-21]
15. Paulo alimaanisha nini aliposali kwamba “roho na nafsi na mwili wenu akina ndugu na vihifadhiwe”? (1 The. 5:23) [w08 9/15 “Neno la Yehova Liko Hai—Mambo Makuu Katika Barua kwa Wathesalonike na kwa Timotheo”]