Ratiba ya Juma Linaloanza Januari 26
JUMA LINALOANZA JANUARI 26
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Mwanzo 17-20
Na. 1: Mwanzo 17:1-17
Na. 2: Kwa Nini Wanadamu Wameshindwa Kuanzisha Serikali Yenye Haki? (rs uku. 265-266 ¶2)
Na. 3: Mungu Ana Jina (lr sura ya 4)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo ya kwenu.
Dak. 10: Jitayarishe Kutoa Mnara wa Mlinzi la Januari 1 na Amkeni! la Januari. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Baada ya kuzungumzia magazeti hayo kwa ufupi, waombe wasikilizaji waeleze makala ambazo zinaweza kuwavutia watu katika eneo lenu na kwa nini zinaweza kuwavutia. Ukitumia baadhi ya makala hizo, waombe wasikilizaji wapendekeze swali ambalo wanaweza kutumia kuanzisha mazungumzo, kisha andiko kutoka katika makala hiyo ambalo wamepanga kutumia kabla ya kutoa magazeti hayo. Malizia kwa kuonyesha jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa, ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4 au mapendekezo mengine yaliyotolewa na wasikilizaji.
Dak. 20: “Je, Unajua Mbinu Zote za Matibabu Yasiyohusisha Damu?”a Ishughulikiwe na mzee. Kwa kumalizia, soma fungu la mwisho. Mahali ambapo hakuna video, zungumzia “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Juni 15, 2004 na Oktoba 15, 2000 au makala “Je! Wewe Uko Tayari Kukabili Hali Ngumu ya Kitiba Yenye Kujaribu Imani?” iliyo katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 1990.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.