Ratiba ya Juma Linaloanza Machi 23
JUMA LINALOANZA MACHI 23
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
lv sura ya 3 ¶1-7, sanduku kwenye uku. 29
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Mwanzo 47-50
Na. 1: Mwanzo 48:1-16
Na. 2: Je, Tumwogope Ibilisi?
Na. 3: Msaada wa Malaika wa Mungu (lr sura ya 11)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo.
Dak. 10: Jitayarishe Kutoa Gazeti la Mnara wa Mlinzi la Aprili 1 na Amkeni! la Aprili. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Pitia magazeti hayo kwa ufupi, kisha uwaulize wasikilizaji ni makala gani ambazo wamepanga kuzungumzia na kwa nini. Ni maswali na maandiko gani yanayoweza kutumiwa kabla ya kumwonyesha mtu makala hizo? Panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa kila gazeti. Katika onyesho moja, onyesha jinsi ya kuanzisha funzo katika ziara ya kurudia. Ikiwa magazeti hayo hayajafika, mabadiliko yanapaswa kufanywa ili sehemu hii izungumziwe wakati magazeti hayo yatakapofika.
Dak. 10: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 10: Onyesha Heshima kwa Kusikiliza kwa Makini na Kufikiria Maoni ya Mwenye Nyumba. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 186-187. Mhubiri mmoja aonyeshe jinsi tunavyoweza kutumia ushauri ulio hapo tunapozungumza na wenye nyumba. Baadaye, waombe wasikilizaji waeleze kwa nini njia aliyotumia mhubiri huyo ni yenye matokeo mazuri.