Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Machi: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi sana kuanzisha mafunzo ya Biblia. Aprili na Mei: Gazeti la Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa, kama vile wale waliohudhuria Ukumbusho na/au mikutano au makusanyiko lakini hawashirikiani na kutaniko kwa ukawaida, jitahidi kuwaachia kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Lengo linapaswa kuwa kuanzisha funzo la Biblia katika kitabu hicho. Juni: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki, wahubiri wanaweza kumwachia kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli, kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, au broshua Mungu Anataka Tufanye Nini?
◼ Wahubiri wanapaswa kupewa matoleo mapya ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! mara yanapofika. Hivyo, watapata nafasi ya kuyasoma kabla ya kuanza kuyatumia katika huduma ya shambani.