Ratiba ya Juma Linaloanza Mei 11
JUMA LINALOANZA MEI 11
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
Nyongeza ya lv kuanzia kichwa kidogo kwenye uku. 209 hadi kichwa kidogo kwenye uku. 212
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Kutoka 27-29
Na. 1: Kutoka 29:1-18
Na. 2: Jinsi ya Kuwa Wenye Furaha (lr sura ya 17)
Na. 3: Hatari za Ushikamanifu Usiofaa
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo.
Dak. 10: Je, Unaweza Kuwa Painia Msaidizi Wakati wa Likizo? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea ukurasa wa 112 hadi 113 wa kitabu Tengenezo. Taja matakwa, na uwaombe wale ambao wameshiriki katika utumishi wa painia msaidizi watoe maelezo kuhusu baraka walizopata.
Dak. 10: Jitayarishe Pamoja na Familia Yako Kushiriki Katika Huduma! Wahoji kifupi ndugu au dada wawili ambao ni vichwa vya familia wanaotumia muda fulani wakati wa Ibada ya Familia kutayarisha familia zao kwa ajili ya huduma. Wanafanya nini ili kujitayarisha, na matayarisho hayo yamewasaidiaje? Onyesha jinsi kichwa cha familia anavyoweza kutumia kipindi cha mazoezi pamoja na familia ili kuwatayarisha kushiriki katika kazi ya magazeti.
Dak. 10: “Fundisha kwa Njia Rahisi.” Mazungumzo kwa maswali na majibu.