Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Septemba: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Inapowezekana, wahubiri watajitahidi kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza mtu anapochukua kitabu. Mwonyeshe mwenye nyumba jinsi kitabu hicho kinavyoweza kumnufaisha kwa kumwonyesha kifupi jinsi funzo la Biblia linavyofanywa. Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mtu akipendezwa zungumzia trakti Je, Ungependa Kujua Ukweli? Ikiwa mwenye nyumba tayari ana trakti hii, mhubiri anapaswa kujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Novemba: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki, wahubiri wanaweza kumwachia kitabu Ibada, au Ujuzi, au kitabu kingine chochote chenye kurasa 192 ambacho karatasi zake zinabadilika rangi au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1995. Broshua Anataka inaweza kutolewa pia. Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Ikiwa kuna watoto katika familia, kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu kinaweza kutolewa.
◼ Hotuba ya pekee ya watu wote katika majira ya Ukumbusho mwaka wa 2010, itatolewa juma linaloanza Aprili 12, 2010. Kichwa cha hotuba hiyo kitatangazwa baadaye. Makutaniko yaliyo na ziara ya mwangalizi wa mzunguko au kusanyiko mwishoni mwa juma hilo, hotuba ya pekee inaweza kutolewa juma linalofuata. Hotuba hiyo haipaswi kutolewa katika kutaniko lolote kabla ya Aprili 12.