Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Ikiwa kuna watoto katika familia, kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu kinaweza kutolewa. Januari: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hicho, basi mtolee kitabu Ujuzi, Mwabudu Mungu, broshua Anataka, au kitabu kingine chochote chenye kurasa 192 ambacho karatasi zake zinabadilika rangi, au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1995. Februari: Toa kimoja kati ya vitabu vifuatavyo: Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Je, Kuna Muumba Anayekujali?, au Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Machi: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Wahubiri wanapaswa kuwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia wanapomwachia mtu kitabu Biblia Inafundisha au ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki nyumbani.
◼ Ukumbusho wa mwaka wa 2011 utafanywa Jumapili, Aprili 17, baada ya jua kushuka. Akina ndugu wanajulishwa mapema ili waweze kufanya mipango ya kutafuta au kukodi majumba mengine ikiwa makutaniko kadhaa yanatumia Jumba la Ufalme lilelile na lazima baadhi ya makutaniko hayo yafanyie Ukumbusho mahali pengine.
◼ Mialiko ya Ukumbusho ya mwaka wa 2010 katika lugha kuu ya kila kutaniko itatumwa hivi karibuni. Ikiwa kuna lugha nyingine katika eneo lenu na mngependa mialiko katika lugha hizo, agizeni mialiko hiyo haraka iwezekanavyo mkitumia Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14). Lugha ambazo mialiko hiyo ya Ukumbusho itapatikana itaonyeshwa katika barua ya kila mwezi inayoonyesha vitabu vinavyopatikana.