Habari Kuu za Utumishi
Kenya: Kusanyiko la Kimataifa la “Endeleeni Kukesha!” lililofanywa katika uwanja wa Moi International Sports Centre, Kasarani, Nairobi, lilikuwa na hudhurio la watu 34,810, kutia ndani wajumbe kutoka nchi 33. Watu 421 walibatizwa. Wote walitiwa moyo sana na programu na pia ushirika wa ndugu kutoka nchi nyingi. Makusanyiko mengine 6 ya Wilaya ya “Endeleeni Kukesha!” yalifanywa baadaye, na watu 12,642 walihudhuria. Watu 152 walibatizwa.
Tanzania: Watu 30,387 walihudhuria Makusanyiko 15 ya Wilaya ya “Endeleeni Kukesha!” mwezi wa Agosti 2009, na watu 421 wakabatizwa.
Uganda: Mwezi wa Oktoba 2009, mapainia wa kawaida 543 walihubiri kwa shangwe na kufundisha kwa bidii. Kila mmoja wao aliongoza kwa wastani mafunzo 6 ya Biblia. Mapainia 129 kati yao walithamini pia pendeleo la kuhudhuria Shule ya Utumishi wa Painia.