Ratiba ya Juma Linaloanza Machi 22
JUMA LINALOANZA MACHI 22
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 1 Samweli 10-13
Na. 1: 1 Samweli 10:17-27
Na. 2: Je, Mwadhimisho wa Krismasi Unapatana na Biblia? (rs uku. 275 ¶3–uku. 276 ¶3)
Na. 3: Je, Nadharia ya Mageuzi Inapatana na Ukristo?
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo. Tia ndani matangazo yoyote yanayohitajika kuhusu Ukumbusho.
Dak. 15: Jitayarishe Kutoa Toleo la Pekee la Aprili 1 la Mnara wa Mlinzi. Pitia yaliyomo katika toleo hili. Waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maswali na maandiko wanayopanga kutumia watakapotoa gazeti hili. Panga maonyesho mawili kuhusu jinsi ya kutoa gazeti hili.
Dak. 15: Wasaidie Wanaopendezwa Ambao Watahudhuria Ukumbusho. Hotuba itolewe na mzee ili kuwakumbusha wahubiri jinsi wanavyoweza kuwasaidia wanafunzi wa Biblia, wahubiri wasiotenda, na wageni wengine ambao watahudhuria Ukumbusho. (Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 2008, ukurasa wa 4.) Panga onyesho fupi kuhusu jambo moja linalotajwa katika toleo hilo. Wakumbushe wote kuhusu ratiba ya usomaji wa Biblia wa Ukumbusho.