Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Mei: Gazeti la Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa, kutia ndani wale waliohudhuria Ukumbusho na/au mikutano na makusanyiko, lakini hawashirikiani na kutaniko kwa ukawaida, zingatia kuwaachia kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Lengo linapaswa kuwa kuanzisha funzo la Biblia. Juni: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hiki, wahubiri wanaweza kutoa kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli, kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, au broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? Julai na Agosti: Wahubiri wanaweza kutumia broshua yoyote yenye kurasa 32 ambayo kutaniko liko nayo akibani. Tumia hasa broshua Mungu Anataka Tufanye Nini?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, na Endeleeni Kukesha! Iwapo kutaniko halina nakala za kutosha za broshua hizo tatu akibani, tumeni ombi mapema.