Habari Kuu za Utumishi
Kenya: Kulikuwa na wahubiri 22,919 katika mwezi wa Machi. Mafunzo mengi ya Biblia yaliongozwa. Kwa wastani, mapainia wa pekee waliongoza mafunzo ya Biblia zaidi ya 9 kila mmoja, mapainia wa kawaida mafunzo zaidi ya 4, mapainia wasaidizi zaidi ya mafunzo 3, nao wahubiri wakaongoza funzo 1 kila mmoja. Bila shaka baadhi ya wanafunzi hao wa Biblia watafanya maendeleo na hatimaye kujiweka wakfu na kubatizwa.
Uganda: Kwa kuwa wanathamini sana upendo wa Yehova na fidia ya Yesu, wahubiri 5,074 walishiriki katika huduma ya shambani mwezi Machi. Walifanya ziara za kurudia 63,972 na wakaongoza mafunzo 12,726.