Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Agosti: Wahubiri wanaweza kutumia broshua yoyote yenye kurasa 32 ambayo kutaniko liko nayo akibani. Tumia hasa broshua Mungu Anataka Tufanye Nini?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, na Endeleeni Kukesha! Iwapo kutaniko halina nakala za kutosha za broshua hizo tatu akibani, tumeni ombi mapema. Septemba: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza. Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mtu akipendezwa zungumzia trakti Je, Ungependa Kujua Ukweli? na ujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Novemba: Biblia—Ina Ujumbe Gani? Habari kuhusu kampeni ya ulimwenguni pote ya kutumia broshua hiyo zitatolewa baadaye. Pia, broshua zifuatazo zinaweza kutumiwa: Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je, Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je, Ziko Kweli?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?
◼ Kuanzia Septemba, waangalizi wa mzunguko watatoa hotuba ya watu wote yenye kichwa “Usiruhusu Macho Yako Yaone Mambo Yasiyofaa!”