Ratiba ya Juma Linaloanza Septemba 20
JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 20
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
cf sura ya 10 ¶18-23, sanduku kwenye uku. 107
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 2 Wafalme 19-22
Na. 1: 2 Wafalme 20:1-11
Na. 2: Kwa Nini Tuwe Wapole? (Mt. 5:5)
Na. 3: Mtu Anawezaje Kumpenda Yehova Ikiwa Anapaswa Kumwogopa Pia? (rs uku. 427 ¶1-2)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo.
Dak. 10: Tulitimiza Nini Mwaka Uliopita? Hotuba itolewe na mwangalizi wa utumishi. Pitia utendaji wa kutaniko katika mwaka uliopita wa utumishi, ukikazia mambo mazuri yaliyotimizwa, na kuwapongeza kwa mambo hayo. Hoji mhubiri mmoja au wawili walio na mambo mazuri yaliyoonwa. Taja sehemu moja au mbili za utumishi ambazo kutaniko linaweza kufanyia kazi katika mwaka wa utumishi unaofuata, na utoe madokezo yanayoweza kuwasaidia kuboresha sehemu hizo za utumishi.
Dak. 10: “Maagizo kwa Ndugu Walio na Migawo Katika Mkutano wa Utumishi.” Hotuba itolewe na mzee.
Dak. 10: Msaidie Mtoto Wako Awe Mhubiri. Mazungumzo yanayotegemea kitabu Tengenezo, ukurasa wa 82. Mhoji mzazi aliye mfano mzuri na ambaye mtoto wake ni mhubiri ambaye hajabatizwa. Alimsaidiaje mtoto wake kufanya maendeleo na kufikia kuwa mhubiri?