Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Septemba: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Jitahidi kuanzisha funzo la Biblia katika ziara ya kwanza. Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mtu akipendezwa, zungumzia trakti Je, Ungependa Kujua Ukweli? na ujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Novemba: Biblia—Ina Ujumbe Gani? Habari kuhusu kampeni ya ulimwenguni pote ya kuitumia broshua hiyo zitatolewa baadaye. Pia, broshua zifuatazo zinaweza kutumiwa: Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je, Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je, Ziko Kweli?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele? Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Ikiwa kuna watoto katika familia, kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu kinaweza kutolewa.
◼ Hotuba ya pekee ya watu wote katika majira ya Ukumbusho mwaka wa 2011, itatolewa juma linaloanza Aprili 25, 2011. Kichwa cha hotuba hiyo kitatangazwa baadaye. Makutaniko yaliyo na ziara ya mwangalizi wa mzunguko au kusanyiko mwishoni mwa juma hilo, yatakuwa na hotuba ya pekee juma linalofuata. Hotuba hiyo haipaswi kutolewa katika kutaniko lolote kabla ya Aprili 25.
◼ Kuanzia juma la Machi 14, 2011, kitabu “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu kitatumiwa kwa ajili ya Funzo la Biblia la Kutaniko. Makutaniko yanayohitaji vitabu hivi, yanapaswa kuviagiza katika agizo lao linalofuata.