Matangazo
◼ Toleo la mwezi wa Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mtu akipendezwa zungumzia trakti Je, Ungependa Kujua Ukweli? na ujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Novemba: Biblia—Ina Ujumbe Gani? Habari kuhusu kampeni ya ulimwenguni pote ya kuitumia broshua hiyo zitatolewa baadaye. Pia, broshua zifuatazo zinaweza kutumiwa: Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je, Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je, Ziko Kweli?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele? Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Ikiwa kuna watoto katika familia, kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu kinaweza kutolewa. Januari: Biblia Inafundisha Nini Hasa? Ikiwa mwenye nyumba tayari ana kitabu hicho, basi mtolee kitabu kingine chochote chenye kurasa 192 ambacho karatasi zake zinabadilika rangi, au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1995.